FARMERS AND COMMUNITY OUTREACH FOUNDATION (FACOF)
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from FARMERS AND COMMUNITY OUTREACH FOUNDATION (FACOF), Njombe.
*CHANJO YA MBEGU*
Agronomist Emmanuel Mwakabana anaandika nakala hii fupi kuwaelewesha wakulima na kuwaongeza ufahamu.
Chanjo ya mbegu ni sumu (kiuatilifu) kinachoongezwa juu ya mbegu. Sumu hii inaweza kuwekwa pia rangi ili kutofautisha mbegu ambazo teyari zimeshakingwa na ambazo bado hazijapata huduma hiyo.
Rangi ambazo utumika sana kwa masoko ya Tanzania kwenye mbegu za mahindi ni *Nyekundu na Kijani*.
Mara baada ya mbegu kuchanganywa na hizi sumu, mbegu hizo zinakuwa hazifahi tena kwa matumizi ya chakula kwa wanadamu ama mifugo.
π Kila pakiti ya mbegu (mahindi, mbogamboga, n.k) ambazo zimeshachanganya na sumu hizi (Seed dresser) uwekwa alama ya ONYO kwenye pakiti. Mfano.
*ONYO*
*Sumu: Mbegu hii imetiwa dawa ya Maxim na Chlorbyriphos. Usiitumie kwa madhumuni ya chakula cha binadamy, mifugo au kukamua mafuta ya kula* tahadhari hii utaiona kwenye mbegu SC 403 Tumbili nyuma ya pakiti.
*SUMU. Mbegu hii imehifadhiwa na dawa na haifai kwa kuliwa au kutumika kuwalisha mifugo au kazi nyingine yeyote isipokuwa kuoanda shambani* Tahadhari hii utaiona kwenye Pakiti ya Mbegu ya Alizeti - Record ya kampuni ya Singidani Seed Company Ltd.
Mifano ya chanjo hizo ni pamoja na...
Maxim
Apron Star
Gaucho
Thirum
Cruiser
Chlorbyriphos nimetaja kwa uchache. Soma vibandiko vya maelezo kwenye pakiti za mbegu utaona mifano mingine ya chanjo za mbegu.
*Kwanini mbegu zinachangangwa ama kupakwa sumu kabla ya kutumika mashambani*.
Yafuatayo ni malengo ya kuchanganya mbegu na sumu tajwa hapo juu.
π Kulinda na kukinga mbegu isibunguliwe na wadudu wa gharani kwa urahisi.
π Kuziongezea uwezo wa uotaji na uchomozaji kutoka kwenye ardhi baada ya kupanda.
π Kuzinginga na magonjwa ya ukungu / kuvu zikiwa katika kuifadhiwa.
Mf. Dumping off, Blight (ukungu)
π Kuzilinda dhidi ya wadudu wavamiao miche katika hatua za awali.
π Kuzikinga dhidi ya kusambaa kwa magonjwa ya ukungu.
π Kudhibiti wadudu wa ardhini waaribifu kwa mazao.
- Minyoo fundo.
Napozitaja kazi hizo tajwa hapo juu sina maana kila sumu iliyochanganywa na mbegu basi inafanya kazi hizo zote; HAPANA.
Chanjo ya mbegu inaweza kufanya kazi moja, mbili ama zaidi kulingana na kiambata amilifu kilichopo kwenye sumu.
Mbegu zinaweza kupata magonjwa, kuvamiwa na wadudu ama mbegu chache kusambaza ugonjwa kwa mbegu zingine.
Ili kutunza na kuakikisha ubora wa mbegu ni vema mbegu zikachanganywa na sumu ili kuakikisha zinabaki katika ubora.
Sumu hizi zinaweza pia kuangamiza magonjwa ambayo teyari yameshavamia baadhi ya mbegu pia kudhibiti uanzishwaji wa vimelea vya kuvu (fungal spores) na kufanya mkusanyiko wako wa mbegu unakuwa salama.
πChanjo za mbegu ni sumu, zaweza kuwa sumu kwa mbegu na hata kwa wanyama na binadamu; hivi matumizi yake yanapaswa kuwa ya umakini na kwa usahihi ili kuepuka madhara.
Umakini huo ni pamoja na kutumia kiasi sahihi cha sumu na kiasi sahihi cha mbegu, na uvaaji wa vifaa kinga wakati wa uchanganyaji wa sumu na mbegu.
*Mfano wa chanjo ya mbegu na namna ya kutumia*
πApron Star 42WS.
βNi chanjo ya uhakika kwa mbegu za mahindi,Soya na Maharage, viazi, pia na mboga mboga.
πSumu hii uchanganywa na mbegu kisha utoa kinga kwa mmea dhidi ya wadudu wote wanaofyonza majani mateke na miche michanga, inzi wa mazao (maharage), inzi weupe, viroboto (Thrips), minyoo ya ardhini (wireworms), panzi (grasshopper), teemites na wadudu wengine.
πPia ni kinga ya magonjwa ya ukungu, kata kiuno (dumping off), ubwiri unga, ukungu, n.k.
πPia uboresha mizizi, na kuwezesha mmea uwe na mizizi mingi na yenye afya.
πUsaidia sana mimea kuota kwa pamoja na kwa kasi na nguvu maradufu.
πPia uzuia matatizo yakuoza mbegu na miziz ama mashina machanga.
πChanjo hii hudumu katika mmea kwa mwezi mzima toka siku ya kupanda mbegu zako.
Upenya kwenye mmea mara baada ya mbegu kupasuka na kuanza kuota.
Hivyo ni kinga yakutosha shambani na hata kitaruni.
Hii ndio maana wataalum tunaita chanjo ya mbegu, ambayo utuakikishia afya ya mazao na ubora wa mavuno yetu.
*NAMNA YAKUTUMIA.*
Changanya 8g za Apron Star na 30 - 40ml za maji changanya vizuri kisha changanya na 4kg za mbegu ( mahindi/soya/Mpunga/maharage n.k) kwenye mfuko ama plastic.
π *Unaweza pia kutumia 5g za sumu hii Apron Star, 20ml za maji na 2kg za mbegu yako (mahindi, Soya, maharage, kunde, mpunga, n.k)*
Acha kidogo ikauke na baada ya kukauka, mbegu hizo zinakuwa teyari zimeshapewa chanjo na teyari kwa kusia/kupanda shambani.
Pia kwa mbegu ndogondogo k**a za vitunguu, hoho, nyanya, pilipili, n.k mchanganyo wake hautahitaji maji na ni kiasi kidogo cha dawa kitaitajika.
Kwa hili nivema kufanya mawasiliano na wataalum kwakua ni ngumu kupata 4kg za mbegu hizi kwa wakulima wadogo wadogo.
Vaa groves wakati wa uchanganyaji epuka kunusa ama kuruhusu hewa ya dawa kuingia puani ama mdomoni. Epuka kushika sumu kwa mikono, hakikisha unavaa mavazi kinga kwa kulinda afya yako.
Ni vema kulinda mwili na afya yako wakati wote unapotumia sumu za kilimo.
Soma maelekezo yaliyopo katika vifungashio vya viuatilifu.
Nimalizie kwa kusema, usipande mbegu bila kuzipa chanjo.
Chanjo itakupa faida nyingi kwa mavuno na afya ya mimea yako.
Ni mimi Bwanashamba nguli.
Agronomist.
Emmanuel Mwakabana.
+255754998944 WhatsApp
ππΎππΎππΎ π π½ πΈ
12/11/2021
karibu
09/02/2021
Karibu tujumuike kwenye kilimo
11/09/2019
Karibuni tulime kitunguu
13/09/2018
*β2 1 N U G G E T Sβ*
*of*
*L I F E*
β1β£β
*Learn to ignore and overlook many things if you truly want happiness in life because the easiest way to a miserable life is to think that everybody is talking about you.*
β2β£β
*Never allow anyone to steal your joy from you.*
β3β£β
*What people say behind your back is none of your business as long as you are true to yourself. Never worry yourself about that.*
β4β£β
*Sometimes minding your own business does not keep people out of your business.*
β5β£β
*No matter your situation in life people will always talk. You can never stop people from talking about you, what you can do is to stop giving them what to talk about.*
β6β£β
*There is a time limit for every rumor in life. Never allow freelance broadcasters put your life on hold. Do what makes you happy. Anyone who cannot feel your pain, has no right to judge you in life. Seventy percent of those who talk bad about you behind your back, wish to be like you.*
β7β£β
*When people can't be like you they try to bring you down and condemn what you have. Those without money will sarcastically say money is not everything in life. (Is poverty anything?)*
β8β£β
*Never allow anyone to put you in a position of depression and self pity in life. Those whose life has no joy will always find every means to remove happiness from other people's life.*
β9β£β
*If there is the GRACE of GOD in your life, then enemies are inevitable. If no one has ever gossiped or talked bad about you, it means nothing good has ever happened to you.*
βπβ
*Never feel bad when old friends become new enemies. They are just tired of pretending to be friends.*
β1β£1β£β
*Never allow the opinions of people who didn't see your tears stop your laughter in life. π¬You don't owe anybody an explanation to be happy.*
β1β£2β£β
*Never see yourself through the eyes of those who don't value you.*
*To be beautiful means to be yourself. To stand out is to be outstanding. You do not need to be accepted by others. You just need to accept yourself.*
β1β£3β£β
*Never beg anyone to accept you for who you are. Anything you acquire through begging will require begging to maintain or retain.*
β1β£4β£β
*Be humble but selective. Being selective doesn't mean you are arrogant or proud. It simply means you know your worth. If you are conscious of your personality avoid too much familiarity.*
β1β£5β£β
*Sometimes when you treat people too much like celebrities, they end up treating you like an ordinary person. You are equally important.*
β1β£6β£β
*Never downgrade yourself while trying to upgrade anybody in life. Anyone who sees you like an option doesn't deserve to be a priority in your life.*
β1β£7β£β
*The dream of a fool is for everybody to become a bloody fool like himself. Avoid negative people if you have a dream. Those without mission will say your vision is just an illusion.*
β1β£8β£β
*Negative minds will never give you a positive life. Anyone who is always reminding you about what is wrong with you has a personal problem which he/she wants to take out on you.*
β1β£9β£β
*Most people spend half of their entire life analysing the faults in other people's life, when their own lives need urgent repairs.*
β2β£0β£β
*Never worry yourself about enemies and friends, because everybody in your life will eventually fall into one of the two categories.*
β2β£1β£β
*Some will hate you and some will love you. Loving you or hating you are both in your favour.*
*When people love you, you live peacefully and happily in their hearts, and when people hate you, you become the landlord in their head living painfully in their brain everyday and giving them sleepless nights.*
β
β β
β
*Be a Blessing to someone*
*Pass it on!*
FAIDA ZA KUNYWA MAJI YENYE NDIMU KILA SIKUππ»
Watalam mbalimbali wa afya wanasema ya kwamba kwa kila siku ni vyema unywe maji ya ndimu ili uweze kujitibu magonjwa yafuatayo;
Unachotakiwa kufanya ni;
Weka maji yenye joto kidogo (vuguvugu) katika glasi au kikombe , kata limao au ndimu vipande viwili na kamua kipande kimoja tu ndani ya glasi yenye maji.
Kunywa na uanze siku mpya. Ni vizuri ukafanya hivi dakika 30 kabla ya kula chochote kingine kwa faida zaidi.
Anza leo kwa kunywa maji yenye ndimu kila siku asubuhi na uone mabadiliko ndani ya mwili wako. Mshirikishe mwenzio ili naye afaidike.
1. Huchochea Mmengβenyo wa Chakula Tumboni
Maji yenye ndimu husaidia chakula kusagika vizuri na haraka katika mfumo wa chakula. Japo limao lina asidi(acid) lakini likiwa tumboni huwa alkali (alkaline) na kufanya mazingira mazuri kwa usagaji wa chakula.
Pia maji ya uvuguvugu husaidia kusawazisha utumbo uliojikunja na kutoa mawimbi tumboni na kufanya chakula kusukumwa vizuri.
2. Huboresha Kinga za Mwili
Vitamini C na potasiumu iliyomo kwa wingi katika limao inasaidia katika utengenezaji wa seli za kinga katika mwili.
3. Husaidia Kinga Dhidi ya Saratani
Vitamini C ni antioksidant (antioxidant) ambayo inasaidia kuondoa free radicalsmwilini ambazo zimetambulika kusababisha saratani (cancer).
Usafishaji wa Mwili na DamuLimao husaidia kusafisha damu kwa kuondoa uchafu. Limao pia husafisha figo ,ini na mfumo wa chakula.
4. Kurekebisha Sukari katika Mwili
Limao husaidia kuweka kiasi cha sukari tumboni na katika mwili kuwa katika kiasi stahili.
Hii inawasaidia sana wagonjwa wa kisukari katika ulaji wao.
5. Dawa ya Kikohozi na Mafua
Limao ikitiwa katika maji ya uvuguvugu na asali husaidia sana katika kutibu mafua na kikohozi kwa njia ya asili.
6. Inasaidia Urekebishaji wa Ngozi na Kupona Makovu
Limao inasaidia kufanya ngozi isizeeke. K**a unataka kubaki kijana basi limao litakusaidia. Tabia za vitamin C za kusafisha uchafu zinasababisha kufanya ngozi kuwa na afya na kutozeeka haraka.
7. Husaidia Kupungua Uzito
Limao hupunguza hamu ya kula. Na inajulikana kuwa sababu kubwa ya watu kuwa na uzito mkubwa ni kula chakula kingi au kula mara kwa mara. Limao litakufanya ujisikie kushiba muda mrefu hivyo kusaidia wale amabao wanataka kupungua uzito.
8. Kuondoa Harufu ya Mdomo
Limao husaidia kuua bakteria wabaya mdomoni ambao husababisha harufu mbaya.
05/06/2018
Mavuna ya parachichi mkoa wa Njombe tayari kwenda ulaya
Click here to claim your Sponsored Listing.
Website
Address
Njombe