Pastor Emmanuel Chatanda
Pastor Emmanuel Chatanda Is The Senior Pastor(SNP) Of Glory Of Christ Church (GCTC) In Ludewa Njombe.
31/05/2026
MUNGU AKIKUBARIKI MJENGEE BWANA
UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
NI UBUNGO PALE.
30/05/2026
UKISHINDA DHAMBI ZOTE NINI KITATOKEA
Amini kwamba pale umeokoka na hutendi dhambi kabisa yaani unaishi maisha matakatifu Sirini na mbele za watu haya ndiyo yatakayo kupata kwenye maisha yako;
1. Mungu wa mbinguni atakuamini na Mungu akikuamini atakubariki kisawa sawa k**a ilivyo kuwa Kwa Ayubu, utafanikiwa sanaa.
2. Mungu atakutumia Kwa viwango vikubwa na kwenye mambo Makubwa katika maisha yako
3. Mungu atakuwa rafiki yako,
Unajua Mungu ni Adui wa dhambi, sasa wewe ukishinda dhambi utaona Mungu anakuwa rafiki yako sana, Mungu akiwa rafiki yako atakutendea mema yote.
4. Uhakika wa kuingia mbinguni ni Asilimia 100%
5. Hapa duniani utamshinda shetani, magonjwa na mapepo yake,
✍️
Mhubiri Kijana
Pastor Emmanuel Chatanda
ANAITWA MR. TANZANIA HAKUNA MTU WA KUMZUIA
MUNGU ANATENDA KAZI KULINGANA NA NAMNA UMEMJUA NA KWA MAJINA YAKE.
30/05/2026
Welcome this Sunday 🔥
30/05/2026
DHAMBI
Dhambi ni kitu Cha ajabu sana huwa inaonekana k**a tamu na inakupa raha unavyo ifanya ila madhara yake huwa ni Makubwa mno mno
Hakuna mtu ambaye anapenda dhambi huu ndiyo ukweli, ila Kuna watu ambao wameshikwa na Dhambi
Mara nyingi utaona baba mzinzi asingependa Binti yake awe Malaya, au mwanae wa kiume awe mzinzi k**a yeye.
Baba mlevi pia huwa hapendi watoto wake wawe walevi japo yeye ni mlevi
Hii inaonyesha hakuna mtu anapenda dhambi.
HII NDIYO TIBA YA KUSHINDA DHAMBI ZOTE
YESU KRISTO
Yesu ndiyo chanzo cha kwanza kitakacho kusaidia kushinda dhambi jumla,
Mtu yeyote ambaye hujaokoka huwezi kushinda dhambi hata iweje
Kumbuka ipo dhambi ya Asili hata k**a utajizuia kutenda dhambi na hujaokoka mwisho wako utakuwa kwenda motoni
Mpokee Yesu Leo Leo.
✍️
Mhubiri Kijana
Pastor Emmanuel Chatanda
29/05/2026
My Dady in the house of the lord.
Bishop Dr. Josephat Gwajima
Isaya 54:17
29/05/2026
UHALISIA WAKO NI UPI?
Usiigize maisha, Moja ya mambo yanayo watesa watu ni kuigiza maisha, usiishi maisha ambayo siyo yako.
Fanya yale tu ambayo unayaweza, ambayo huyawezi achana nayo
Ukiifahamu nafasi yako ni ipi fanya Kwa bidii na ubora hapo hapo ulipo.
Mungu ni wa hatua Kwa hatua, usikwepe mchakato kwenye kitu chochote unachofanya.
Shortcut nyingi huwa zinaishia kwenye uharibifu.
Mambo yote ya haraka haraka, huwa ni ya shetani ambayo ukiyafanya unaangamia.
Shetani husema nitakutajirisha haraka, nitakupa majumba na magari haraka, utakuwa maalufu haraka.
Waswahili wanasema, " HARAKA HARAKA HAINA BARAKA"
K**a unataka ufanikiwe kubariana na hatua uliyo nayo sasa ikiendelea kuamini kuwa utakuwa na hatua kubwa siku zijazo.
Kamwe usivunjike moyo amini tu na Kwa hakika utafika.
N.b Maisha ni safari ndefu Kila kipindi unachopitia Toka na somo, na uendelee mbele.
✍️
Mhubiri Kijana
Pastor Emmanuel Chatanda
24/05/2026
Siku za Kupenya 28.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the place of worship
Website
Address
IBANI, Ludewa
Njombe