Kitambo Inspiration
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Kitambo Inspiration, Writer, Isamilo, Mwanza.
Ukrasa huu ni mahususi kwa :
⛪Uchambuzi wa Neno la Mungu(Biblia)
🏧Masomo ya kuhamasishana kiuchumi na kiroho
💽Video au short clips za mahubiri ama maigizo kuhusu injili na uchumi.
#Karibuni sana wana wa Mungu@Follow page hii na kushare posts
16/06/2026
MDAU ALALAMIKIA MAHUBIRI YA WASABATO
Shalom wapendwa
Kuna mdau mmoja kutoka ngara alinipigia simu jana akanieleza kuwa yuko nyakahura mzani hapo wasabato wameweka kambi ya mkutano wa injili lakini cha kushangaza wanachozungumza hakiwezi kuwasaidia watu na wala sio injili ..
Akasema
1.wamekuwa wakipondea kanisa katoliki vibaya mno kuwa limepotoka na lilihamisha sabato kuwa jumapili..
2.wamekuwa wakihubiri mambo ya vyakula
MY TAKE
1.Ni wapi Yesu au mitume wake walienda kuhubiti kuhusu siku ya kuabudu??
2.Hivi siku ya kuabudu inamsaidiaje mlevi? Muuaji? Mwizi??
3.kwanini wasabato hawahubiri wokovu na ujazo wa Roho mtakatifu ..wamekazana siku ya sabato na vyakula?
BAADA YA KUHUBIRI SIKU YA KUABUDU
Tangazeni wokovu wa Yesu ...mtu akimwamini Kristo ndipo mambo ya taratibu na ratiba za ibada Ndipo hufundishwa...
mwone Yesu alihubirije??
Marko 1:15
[15]akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili.
And saying, The time is fulfilled, and the kingdom of God is at hand: repent ye, and believe the gospel.
Mitume walihubiri nini??
Matendo ya Mitume 2:38
[38]Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
MITUME WALIHUBIRI
1.Yesu ni mwokozi wetu tunapaswa kumwamin yeye
2.kutubu dhambi na kubatizwa
3.kupokea kipawa cha Roho mtakatifu.
Injili isiyohubiri wokovu wa Yesu ni batili.
Injili isiyohubiri ubatizo wa Roho mtakatifu hiyo ni batili..
Asanteni kwa wale mlio mlionielewa.
Wagalatia 1:6-8
[6]Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine.
[7]Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo.
[8]Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe
10/06/2026
UMEDANGANYWA NA WA SDA NAOMBA NIKUSAIDIE RAFIKI YANGU
Shalom wapendwa
Kwa Leo naomba nimsaidie rafiki yangu huyu na yeyote mwenye fikra k**a hizi..
Katika ujumbe wake alioutoa ameeleza kwamba Bwana wa sabato anakuja na ili tuwe salama tunapaswa kushika sabato ndo mhuri wake..
Akatoa maandiko ..Ezekieli 20:20, kum31:15-18, isaya58:13-14 nk
SASA TWENDE SAWA
1.kosa kubwa ambalo linawatesa wasabato na litaendelea kuwatesa ni kushindwa kutafsiri mkutadha ..yaani ujumbe mkuu , lini? Kwetu tufanye nini nk
Kwahiyo wao wanachukua kamstari kamoja tu na kutembea nako ...Imesalia raha ya sabato... Au sabato imefanyika kwa wanadamu...
2.katika maandiko hayo aliyotaja hakuna hata moja la agano la jipya..ndio maana nilisema hawa wasabato wanajifanya kumtukuza Kristo lakini ihalisia wamefungamana na mafundisho ya misa
3.Agano jipya limeweka wazi kwamba mhuri wetu ni Roho mtakatifu...
Sasa hawa jamaa unaweza kujiuliza kwanini hawataki kumnadi Roho mtakatifu?? Ilihali Yesu anaondoka atakuja msaidizi ROho mtakatifu ...yohana14:26
Na pia paulo natuweka bayana kwamba mhuri wetu tunaupata kwa Roho mtakatifu..si kwa kusali siku ya jumamosi..AMKENI
Waefeso 4:30
[30]Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi.
4.Jambo la kujiuliza dogo sana ..kwamba k**a sabato ingekuwa lazima au mhimu kiasi hicho k**a wanavyotuelezea ndugu zetu wasabayo ...
Kwanini Yesu hakuna mahali aliagiza au kusiaktiza wafuasi wake kuishika sabato??
Baada ya ukristo kuanza nyaraka nyingi zilizoandikwa na mitume ...za Paulo, yo ha na, petro ,yuda nk kwanini hakuna hata mmoja aliyewakumbusha au kuwasisitiza kuishika ??
K**a ingekuwa mhimu au lazima kwa wakristo naamini wangesisitiza ...
Mbona sheria zingine au amri zingine k**a :usiibe , usiabudu sanamu, usizini nk zimeagizwa kwa wakristo na Yesu au nyaraka za mitume lakini hakuna agizo la kuendelea kushika sabato?? Je Walijisahau ? Walipuuza??
AMKENI AMKENI AMKENI
Mungu awabariki
09/06/2026
MAKOSA TANO YA WASABATO
Shalom wapendwa
Haya ni makosa niliyobaini kwa wenzetu wasabato.
1.Wanajihesabia haki
Yaani wanaamini kabisa kwa kusali jumamosi kwao basi mlango wa kuingia peponi ni wao..na asiyesali jumamosi ni jehanamu tu.
Na wanaamini kwa kusali jumamosi na mafundisho ya Elwn gwhite wako sahihi kabisa na hawana haja ya kujifunza tena
2.wanajiita wakristo lakini wamekumbatia agano la wayahudi
Hoja zao zote si kutetea injili ya Kristo bali kutetea agano la wayahudi.Hawako katika fungamano la agano jipya
3.Wanatetea sabato kuriko Bwana wa sabato
Ukiwafuatilia utabaini kwamba wanahubiri zaidi sabato kuriko kazi ya msalaba.
4.wanang'ang'ania kushika sheria kuriko kushika neema
Ndio maana nguvu na madhihirisho ya Roho mtakatifu hayapo.
5.Wamewekeza katika sheria za mwili zaidi kuriko mambo ya rohoni k**a vyakula ,sabato nk
..Mungu awabariki sana ..
Unaweza ongezea na wewe pia..
Upendo mkubwa hupimwa kwenye matatizo makubwa
04/06/2026
KIGOMA MWAKEYE TUMEWAFIKIA
04/06/2026
Usihukumu watu kwa makosa yao ya jana ,watu hubadilika ,watu huinuka tena upya na kufanya vizuri
Wanaokudharau Leo kesho watakudharau tena ukiacha kufanya mambo ya msingi..fanya mambo ya msingi utengeneze heshima ya kesho..@
NJIA yenye nguvu ya kulipa kisasi kwa mtu aliyekukosea ni kusamehe..
Warumi12:19-21
Nakusihi kwa jina la Yesu samehe wote ...
Moja ya njia ya uhakika ya kudumbukia kwenye umaskini ni kujifanya tajiri ilihali bado masikini NEW ERA PROGRAM
28/05/2026
NGUVU YA KURIDHIKA
Shalom wapendwa ..
Hongereni na mapambano ..lakini poleni nimekuwa offline sana kwasababu ya majukumu kadhaa..
Lakini leo Natamani kushare na nyinyi hiki kitu ..nguvu ya kuridhika..
1 Timotheo 6:6
[6]Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa.
Maisha yamejaa mahitaji mbalimbali na mambo mengi mazuri na kwa kweli ni haki yetu kuwa na kila kitu kizuri..lakini mhubiri anatuambia kila jambo lina nyakati na majira ..
Mhubiri 3:1,4
[1]Kwa kila jambo kuna majira yake,
Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
[4]Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;
Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
Ndio kuna wakati wa kupitia magumu na huzuni kuna wakati wa kuburudishwa na Bwana..
Kuna wakati wa kudharauliwa na kuna wakati wa kuheshimiwa...
Suluhisho hapa ni kutambua wakati uliopo kisha UKARIDHIKA yaani ukakubaliana na hali uliyoanayo hata k**a ni duni ,mbaya ..
Ninaposema kuridhika si kuacha kupambana bali kukubaliana kwa muda na hali duni uliyonayo huku ukipambana chini kwa chini kufikia viwango unavovitamani..
Isaya 40:29-31
[29]Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.
[30]Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;
[31]bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa k**a tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
Ndio ridhika na hali uliyonayo huku ukingoja wakati wa kuinuliwa na Bwana...usijiumize kwa maswali mengi yasiyo na majibu ..usiishi kwa huzuni kwasababu ya hali uliyo nayo...
An za kufurahia maisha uliyo nayo hata k**a ni duni kwani ipo kesho ya kuinuliwa kwako ya kuondolewa maumivu na simanzi..
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the public figure
Telephone
Address
Isamilo
Mwanza