First care Tz
Kalibu Account ya First Care Tz kwa Habari za
Kimataifa & Kitaifa
Michezo
Historia za watu na vitu
Facts
Celebrity news
Science & technology updates
02/05/2020
Je, Wajua?
Kariakoo inatokana na neno la kiingereza "carrier corps", Hiki kilikua kikosi cha wapagazi waliobeba mizigo ya wanajeshi wakati wa vita kuu ya kwanza. Jina hilo kwa Kiswahili lilitamkwa karia- koo na liliendelea kutumika hivyo hadi leo.
02/05/2020
Je, Wajua?
Jina Muhimbili limetokana na neno la Kizaramo "mibili" likimaanisha kiungo cha mtoto tumboni kwa mama (plasenta) Hospitali ilipoanza Wazaramo walisema "Hapo ndipo wamama wanaenda kuacha mibili yao" Muhimbili likazaliwa hivyo, nalo ladumu hadi leo.
24/02/2020
Mtandao wa Facebook umeweka utaratibu wa kuwalipa watumiaji wake kwa kusoma kurasa za maandishi kwa sauti, ili kuimarisha mfumo wake wa utambuzi wa sauti. Zoezi hilo linachukua dakika tano likiwa na jumla ya pointi 1000 ambapo ukikamilisha unalipwa Dola 5 (Sh.11521).
21/01/2020
Katika geleza hilo kulikuwa na Chumba kimoja Chumba hicho kilijulikana k**a "Marital Prisons." wanandoa wanaotaka kutengana walipaswa kufika kwa mchungaji wa eneo hilo.
K**a uamuzi wao ulikua kutengana basi walifungiwa kwenye hicho chumba kwa muda wa Wiki sita, ndani ya chumba hicho kulikua na, kitanda kimoja cha kamba tena kidogo, kiti kimoja, meza moja na kabati moja Na Couple ilipaswa kutumia hivyo vitu wote kwa pamoja.
Kwa hivyo, wanandoa iliwalazimu kupatana haraka iwezekanavyo, ili waweze kutoka nje ya gereza na kurudi nyumbani kuendelea na kazi zao.
Kusudi la kifungo hiki lilikuwa kuwapa wenzi hao nafasi ya kumaliza tofauti zao. Talaka inaweza kutolewa ikiwa tu, hatua hii haikufanikiwa.
Chumba hicho kilibuniwa mnamo karne ya 15 ili kupunguza wimbi la Talaka Maeneo hayo.
Kwa sasa Hicho chumba hakitumiki na badala yake kipo chini ya UNESCO k**a urithi wa dunia.
Lakini watu wengi wanapendekeza kirudishwe tena kwani kingesaidia sana dunia ya leo. .
Tagi mshikaji wako ambaye iliaweze kupunguza uzito lazima awe na mwalimu k**a huyu πππ
29/11/2019
Leo inatimiza miaka 120, tangu ilipoanzishwa Novemba 29, 1899.
Iliasisiwa na kundi la wanasoka wa Kiispaniola, Kiingereza na Kiswisi wakiongozwa na Joan Gamper (akiwa na miaka 22). BarΓ§a ni moja ya timu 3 anzilishi za La Liga, pamoja na Athletic Bilbao & Real Madrid.
29/11/2019
Utawala mpya wa Sudan umeamuru kuwa chama cha kiongozi wa kiimla aliyeondolewa madarakani Omar al-Bashir kivunjwe na utawala wake "usambaratishwe", ukiitikia mwito wa waandamanaji ambao kampeni yao ilisababisha kuangushwa kwa kiongozi hiyo.
Bashir na chama chake cha National Congress - NCP aliiongoza nchi hiyo ya Afrika Kaskazini tangu mwaka wa 1989 kabla ya vuguvugu la maandamano ya kitaifa kumuondoa madarakani mapema mwaka huu.
Baraza jipya la uongozi nchini humo na baraza la mawaziri likiongozwa na Waziri Mkuu Abdalla Hamdok limefanya uamuzi wa kukivunja chama, kwa kuidhinisha sheria iliyoitwa "kuusambaratisha utawala wa Juni 30 1989."
Amesema k**ati itaundwa ili kuk**ata mali zote za chama hicho. Waziri Mkuu huyo amesema hatua hiyo sio kulipiza kisasi dhidi ya watawala wa zamani wa nchi hiyo, bali ni kudumisha hadhi ya watu wa Sudan ambayo ilichafuliwa na watu wasio wakweli.
29/11/2019
Naibu Waziri wa Kilimo, ametisha kikao cha dharura cha Bodi ya Pamba Shinyaga, mabenki na wakuu wa mikoa inayolima pamba, na kuagiza ifikapo Desemba 8, 2019 madeni yote ya pamba yawe yamelipwa na wakulima wakopeshwe mbegu kwani hawawezi kununua na wengi hawajalipwa.
29/11/2019
Mkufunzi wa Arsenal Unai Emery amefutwa kazi baada ya kuongoza timu hiyo kwa kipindi cha miezi 18, hiyo ni kufuatia muendelezo wa matokeo mabaya.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Telephone
Website
Address
Mwanza