Mlewa Electronics

Mlewa Electronics

Share

Ndani ya page hii ya MLEWA ELECTRONICS utaweza kufahamu MAMBO YOTE ambayo HUJAWAHI kabisa kuyaskia h

25/11/2022

HII NDO QATAR NA UCHUMI WAKE:

WANASEMA ni nchi ya mfalme na mwanawe. Hawapotezi muda kwenye malumbano ya siasa!

QATAR ilipata uhuru mwaka 1971 kutoka kwa mwingereza. Ni nchi inayoongozwa na mfalme. Kumbe mambo yasipoenda hata mfalme hutumbuliwa. Alianza Ahmad Al Thani baada ya uhuru. Mwaka 1972 alipinduliwa na mjomba wake Khalifa Al Thani. Huyu alipinduliwa na mwanawe prince Hamad Al Thani mnamo mwaka 1995. Prince Hamad aliachia madaraka kwa Tamim Hamad Al Thani mnamo mwaka 2013. Ukoo huo wa Al Thani hauruhusu ukoo mwingine kuchukua madaraka na hakuna chama cha siasa hata kimoja. Baraza la mawaziri huchaguliwa na kutumbuliwa wakati wowote mfalme akiamua.

UCHUMI wa Qatar unategemea mafuta. Kampuni ya serikali ya Qatar Petroleum (QP) inasimamia utafiti, uchimbaji, usafishaji, usafirishaji na kuhifadhi mafuta. Mwenyekiti wa kampuni hiyo pia ni waziri wa nishati na viwanda. Mafuta na gesi vinatoa asilimia 60 ya kipato cha Qatar.

MAISHA ya waqatari yanategemea kipato cha mafuta ya Qatar. Serikali inaweza kuwapa waqatari huduma za maji, afya, mpaka nyumba bila ya malipo. Elimu ni bure. Wanafunzi wanapata chakula shuleni. Wanasafiri bure, hata nguo wanapewa bila ya malipo. Vilevile serikali inalipia wanafunzi wasomao nje ya nchi. Kuna habari kutoka kwa wenyeji kuwa mqatari hata akiwa hana kazi analipwa mshahara kila mwezi.

ZOEZI hilo linawawezesha waqatari kuachia wageni kazi nyingi huku wenyewe wakiwa wanashikilia nyadhifa muhimu hasa kwenye kazi za serikali. Waafrika hasa kutoka Misri, waasia, wazungu ni katika orodha kubwa ya wafanyakazi wa kigeni nchini humo. Wakenya wanajiona tamu sana Doha airport, k**a vile wako Nairobi. Waajiri ni wakali kwenye mikataba na kubana wafanyakazi hasa kwenye masuala ya kubadilisha kazi.

UTAIFISHAJI wa mafuta ulifanywa kwa awamu. Mafuta yaligunduliwa kwenye miaka ya 1950. Mwanzoni mafuta yalimilikiwa na kampuni ya British Petroleum (BP) na baadhi ya makampuni ya Iran. Wakati huo serikali ilikuwa ikimiliki asilimia 25, huku hisa zikiongezeka kidogo kidogo kila mwaka. Kufikia mwaka 1975 serikali ilishavunja mikataba ya awali. (kwa staili ile ya Acacia) Na kuanzia mwaka 1976 kampuni ya Qatar Petroleum imekuwa ikimiliki mafuta ya Qatar kwa *asilimia 100.* Sambamba na utaifishaji huo vituo vya kuuzia mafuta, teksi, mabasi na treni vinamilikiwa na serikali. Uber na teksi bubu zipo lakini ni marufuku kufika maeneo muhimu k**a uwanja wa ndege.

UTALIPENDA jengo la makao makuu ya kampuni ya QP. Ni mnara mrefu sana wa bluu uliopanda ki-New York. Chini kuna k**a tufe kubwa lenye maandishi ya Qatar Petroleum na juu ya gorofa hilo kuna kibaraza kinachozunguka usiku huku kikiwa na maandishi ya bluu yanayosomeka *QATAR PETROLEUM .* Ikiwa ni uthibitisho tosha kuwa kinachoendelea ndani ya jengo hilo ni mafuta ya Qatar tu.

SHIRIKA la ndege la Qatar pia linamilikiwa na serikali. Lina ndege kubwa za aina ya Boeing na Airbus zaidi ya 320. Ni ndege mpya za kisasa nyingine zina uwezo wa kuweka na kuondoa kivuli kwenye madirisha. Qatar hawana vivutio vingi vya utalii lakini ndege hizi hubeba watalii wengi waendao Afrika ya mashariki. Wanajaza ndege ya watalii kutoka Doha mpaka Kilimanjaro, halafu wanawarudisha kutoka Kilimanjaro kwenda Doha kwa kupitia Dar-es-salaam. ATCL wajipange vizuri na mtihani huu. Vilevile huduma za shirika hili ni nzuri sana. Achana na mashirika ya ndege za wazungu wanabania chakula. Qatar airways wanakupa mpaka chapati.

MIPANGO miji ya Qatar ni ya kukata na shoka. Si Ulaya si Marekani wanaowafikia. Waarabu hawa wana taa za barabarani zenye mwanga wa maua kwenye mlingoti mzima wa taa. Hakuna mashimo barabarani, na wana magari ya kifahari mno. Sio city k**a Tanga ni Metropole. Wana masoko na maduka ya kisasa likiwemo lile wanaloliita Villagio. Juu ya soko hili wamechora rangi ya mawingu inayofanya mtu akiwa ndani aone k**a anatembea nje. Mjengo wa aina hii hupatikana sehemu chache duniani ikiwemo Las Vegas, Johannesburg na Macau. Mahoteli yao ni ya kimataifa na ya hadhi za juu.

UWANJA wa ndege wa Doha ni mkubwa, unavutia na wa kisasa. Umbali wa kutokea temino mpaka kwenye ndege kuna mama wa kizungu aliuliza k**a safari ni ya basi au ya ndege. Boeing tano au sita za Qatar zinaweza kujipanga mstari zikisubiri zamu ya kuruka. Inawezekana ni uchache wa ardhi lakini huu uwanja huu umejengwa kwa kufukia mchanga baharini.

HALI ya hewa si nzuri k**a ya Tanzania. Waqatari wako jangwani. Joto la nyuzi 108 f, 44 (c) ni kawaida wakati wa majira ya joto. Ukitaka upate uhalisia wake ingiza kichwa kwenye oven. Lakini wanalimudu joto hili. Nyumba zao hata kwenye masoko kuna mizizimo ya viyoyozi usawa wa winter kali.

*KILIMO* kimewatupa mkono kutokana na kuwa jangwani. Wana mashamba machache ya ngano na tende. Lakini hakuna wanachokosa. Ukitaka kujua tofauti ya nyama za plastiki za MacDonald na nyama ya ukweli agizia mpunga na nyama Doha. Halafu kakae bichi ule biriani yao hawa jamaa.

WENYEJI ni waislamu na mavazi ya kiislamu yametawala barabarani. Misikiti huanz kuadhini saa tisa za usiku. Hawana uislamu ule wa kushikana mashati. Wageni wanachotakiwa ni kuzingatia sheria za msingi za nchi. Kwenye ndege zao na maduka yao hasa ya uwanja wa ndege wanauza pombe tena hata zike kali. Hata hivyo ndani ya ndege zao una chaguo la kusikiliza Quran badala ya kuangalia movie au vipindi vya televisheni. Vibaka barabarani wala hofu ya kutapeliwa hakuna.

MAJAHAZI ya kizamani yale ni kivutio kikubwa baharini. Usiku yanawaka mataa na kutembeza watalii baharini kwa malipo.

WANA mafuta na jangwa.

*PENGINE* walianza maendeleo zamani. La hasha, Qatar ni nchi changa kuliko nchi nyingi za Afrika. Ilipata uhuru mwaka 1971. Picha za Doha ya 1970 na picha ya Doha ya leo, tofauti yake ni k**a usiku na mchana.

KUBWA walilolifanya ni kumiliki kikamilifu rasilimali yao moja waliyopewa na Mungu.

0766 1995 64

25/11/2022

Hapa sidhani k**a fundi mwenzangu alipewa posho ya kazi, kazi ngumu hii.

10/10/2021

JE WAJUA?* *JUA SASA!! 👇

WAJUE WATUMIAJI 10 WA KWANZA WA "FACEBOOK".
_________________________

*USISAHAU KU LIKE PAGE YETU, ILI UPATE KUJUA MENGI ZAIDI KILA SIKU.

*FACEBOOK* Ni mtandao wenye watumiaji takribani bilioni 1.9+ kila mwezi na unaoshika nafasi ya kwanza kwa kuwa na watumiaji wengi zaidi duniani kwa mwaka wa 12 mfululizo. Swali linalotia mzuka ni nani na nani walikuwa watumiaji 10 wa kwanza wa mtandao huu? Ipo wazi kabisa kuwa Mark ndio alikuwa mtumiaji wa kwanza kabisa, ila je wa pili, watatu wanne na watano alikuwa nani.

ID namba za kwanza za mtandao huu hazikuwa zinafuata mlolongo kamili, k**a mmiliki na mtumiaji wa kwanza wa mtandao huu Mark Zuckerberg ana ID ya 4.

Haya sasa hawa ndio watumiaji 10 wa kwanza wa mtandao huu.

⬛ *1. Mark Zuckerberg (ID – 4):*

Mark Zuckerberg (ID – 4):mtu wa kwanza kuwa na akaunti katika mtandao huu. Mark Zuckerberg alitengeneza mtandao akiwa chuoni Havard na alijipa ID namba 4 kwakuwa tatu za mwanzo alikuwa amezipoteza katika majaribio. Mark ana mtoto mmoja anayeitwa Max aliyezaa na mchumba wake wa muda mrefu Priscilla Chan.

⬛ *2. Chris Hughes (ID – 5):*

Huyu ni mtu wa pili katika orodha wa wagunduzi wa mtandao huu akiwa na namba 5 k**a ID yake.Ni mhitimu wa chuo cha Havard na alihudumu k**a msemaji wa Facebook mpaka mwaka 2007 alipoamua kumuunga mkono Obama katika kampeni zake za Urais.Kwa sasa Hughes ni Mkurugenzi na Mhariri Mkuu wa gazeti la chama cha Republican The New Republic magazine.

⬛ *3. Dustin Moskovitz (ID – 6):*

Bwana Dustin alikuwa room mate (mwanachumba) wa Zuckerber kipindi wapo chuo na ni mmoja ya watu walioanzisha mtandao huu kwa mara ya kwanza. Zuckerberg alimpa Moskovitz kazi ya kuziba mianya ya usalama katika facebook baada ya kusoma PHP kwa muda mfupi tu. Alikuwa makamu wa rais wa wahandisi wa mtandao huo kabla ya kutimua Facebook akiwa na rafiki yake Justin Rosenstein mwaka 2008 na kwenda kutengeneza Asana.

⬛ *4. Arie Hasit (ID – 7):*

Alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kuwa na akaunti katika mtandao huu japo hakuwa mmoja wa wagunduzi wa mtandao huu. Akiwa Havard alikuwa akisoma shahada ya historia ya mambo ya Israel na baadae alirudi Jerusalem na kufundisha katika chuo kwa kujitolea elimu ya dini na maadili ya Wayahudi.

⬛ *5. Andrew McCollum (ID – 26):*

Huyu ni mmoja wa waanzilishi wa mwanzo kabisa wa mtandao huu aliyekubali kuacha chuo ili afanye kazi na Facebook. Alirudi chuo baadae mwaka 2007 kumalizia shahada ya Kompyuta Sayansi hapo hapo Havard. Kwa sasa ni CEO wa kampuni ya Philo inayojihusisha na usambazi wa Cable Tv katika vyuo nchini Marekani.

⬛ *6. Colin Kelly (ID – 27):*

Huyu ni mtaalamu wa masuala ya Fizikia katika chuo kikuu cha Havard aliyekuwa akijihusisha zaidi na tafiti za kinyuklia chuoni hapo. Baadae alipata shahada ya sheria katika chuo cha Columbia University School of Law, na akajipatia umaarufu sana katika kesi ya kibaguzi iliyohusisha taifa la Marekani na Windsor. Kwa sasa anashi jijini New York.

⬛ *7. Mark Kaganovich (ID – 28):*

Kaganovich alikuwa mtaalamu wa mambo ya kemia na biolojia katika chuo cha Havard na alikutana na Zuckerberg katika darasa la Hesabu, pia walikuwa wakikutana katika mabweni ya chuo hicho. Anakumbuka kipindi bwana Zuckerberg alipokuwa akimlazimisha kuweka profile picture yake kwani alikuwa mzito kidogo kufanya hivyo.

⬛ *8. Andrei Boros (ID – 29):*

Huyu pia alikuwa mtaalamu wa mambo ya Uchumi katika chuo hicho cha Havard. Kwa sasa anafanya kazi katika kampuni ya CapeView Capita huko jijini London.

⬛ *9. Manuel Antonio Aguilar (ID – 30):*

Kwa sasa jamaa huyu ni Rais wa kampuni inayojihusisha na ujenzi wa nyumba za kuishi za bei nafuu, ya CASSA (Construcción AutoSuficiente, S.A)

⬛ *10. Zach Bercu (ID – 31):*

Mtaalamu wa mambo ya miale ya kinyuklia anayefundisha katika chuo cha Emory University School of Medicine, alihitimu magna cm laude katika psychology pale Havard kabla ya kwenda kuongeza elimu katika chuo cha Emory University.



Tv Simu Computer Radio N.k

09/10/2021

UJUE MWISHO WA DIKTETA ALIYEITIKISA LIBERIA, "SAMUEL DOE."_*

Huyu ndiye SAMUEL KANYON DOE rais aliyeuawa kikatili sana nchinii Liberia,,,,,,
Samuel Kanyon Doe alizaliwa May 6, 1951 jijini Tuzon, nchini Liberia...
Alfajiri ya Aprili 12, 1980, kikundi kidogo cha wanajeshi 17 kilijipenyeza ndani ya makazi ya Rais jijini Monrovia... Ikulu walimkuta Rais William Tolbert bado amelala... Wakamuua... Aliyeongoza kikundi hicho alikuwa askari kijana na wa cheo cha chini, Sajenti Samuel Doe...
Na inasemwa kuwa Doe alipoingia Ikulu na wenzake, alidhani watakwenda kumlalamikia Rais juu ya mishahara midogo ya askari wa vyeo vya chini... Lakini jinsi walivyoikuta Ikulu ikiwa nyepesi vile, ndivyo mipango ilipobadilika na kuamua kumuua Rais mwenyewe na kuchukua madaraka...
Samuel Doe alikuwa askari ambaye hata madarasa manne ya shule ya msingi hakuyamaliza... Alitoka kabila dogo la waishio misituni, kabila la Krahn... Ni watu wa kabila k**a lake, masikini na ambao ndio waliotoka vijijini na kukimbilia jijini Monrovia kutafuta vibarua na pesa... Kwa wenye bahati, k**a Samuel Doe, walionekana mitaani na kuitwa kujiunga na Jeshi...
Na k**a ilivyokuwa kwa Idi Amin, Urais ulimdondokea tu Samuel Doe, k**a vile mtu aliyeshinda bahati nasibu...
Ujio wa Samuel Doe uliwafaya WaLiberia waamini kuwepo kwa mabadiliko... Kuondokana na utawala wa kifisadi na kirasimu wa William Tolbert...
Samuel Doe akajitangaza kuwa Rais, April 12, 1980... Haraka sana akawatwanga risasi mawaziri wote wa Tollbert... Ni kwenye pwani ya bahari huku wananchi wakitazama k**a mechi ya mpira...
Sajenti Samuel Doe akatawala kwa kipindi cha miaka kumi... Nchi ikawa k**a imesimama....
Watu wa kabila la Samuel Doe waliogopewa na makabila mengine… Waliweza kufanya lolote lile na hakuna aliyewagusa… Waliua na waliwatisha wengine... Wengi wasio wa kabila la Rais Doe, waliishi kwa hofu kubwa…
Na kile ambacho kila mtu asiye wa kabila la Doe, alikuwa anakisubiri, ni kushuhudia mwisho wa Sajenti Samuel Doe…
Na hapa akatokea Charles Taylor… Huyu alikuwa rafiki wa zamani wa Sajenti Samuel Doe...
Lakini, urafiki wao ulikufa pale Samuel Doe alipodai kuwa Charles Taylor alimtapeli dola milioni moja… Kisha Taylor akatorokea Marekani… Huko akaanza kufanya biashara kwa mtaji wa fedha alizomtapeli Sajenti Samuel Doe…
Charles Taylor naye akaishia gerezani nchini Marekani kwa mashtaka ya utapeli… Lakini akatoroka jela na kukimbilia Ivory Coast... Na akiwa Ivory Coast, Charles Taylor akaanza kujipanga kwenda kuuangusha utawala wa Sajenti Samuel Doe… Charles Taylor akiwa Ivory Coast, alikiandaa kikosi cha wapiganaji 60… Kikosi kilikuwa tayari kwa kuingia Monrovia kumwondoa Samuel Doe madarakani…
Ilikuwa ni mwaka 1989… Wakati huo, wajuzi wa masuala ya kijeshi waliamini kabisa, kuwa Sajenti Samuel Doe angeweza, kirahisi kabisa, kumteketeza kijeshi Charles Taylor na kikosi chake cha watu 60… Sajenti Samuel Doe angeweza kufanya hivyo hata kabla Charles Taylor hajavikaribia viunga vya Monrovia…
Badala yake, ‘’Master Sergeant’’ Samuel Doe, aliwatuma mstari wa mbele, wanajeshi kutoka kabila lake la Krahn... Ni wanajeshi wa kuokoteza ambao wengine hawakuwa hata na viatu… Wanajeshi wale wa Samuel Doe, njiani wakitokea mji mkuu Monrovia wakielekea uwanja wa mapambano, wakaanza kufanya wizi wa ngawira, kuiba mali za watu…
Habari za askari ‘’vibaka’’ wa Samuel Doe zikasambaa haraka kwenye vijiji vya msituni…
Huko watu wakajitolea kujiunga na vikosi vya Charles Taylor kukabiliana na askari wa Samuel Doe…
Jeshi la Taylor likakua kwa haraka… Baada ya miezi sita tu, likaingia kwenye viunga vya mji mkuu wa Liberia, Monrovia, June 1990…
Ndipo hapo kwenye kambi ya Charles Taylor ugomvi ukazuka… Nani atakuwa Rais???... Nani atakuwa na mamlaka ya hazina kuu???... Ni ugomvi uliowatenganisha Charles Taylor na Prince Johnson aliyeamua kuachana na Taylor na yeye kuanzisha kikosi chake…
Wote wawili walikuwa na tamaa ya Ikulu. Vita sasa ikawa ya vikosi vitatu kugombania kuingia Ikulu ya Monrovia: Kikosi cha Sajenti Samuel Doe kinachojihami, kikosi cha Charles Taylor na kikosi cha Prince Johnson... Wote wakaanza kupigana wenyewe kwa wenyewe kugombania Ikulu ya Monrovia…
Mitaa ya Monrovia wakaonekana askari wa makundi tofauti wakipigana. Hata watoto waliingizwa kwenye vita vile vya kiwendawazimu…
Hatimaye, mwishoni mwa mwezi August 1990, vikosi kutoka nje viliingilia mgogoro ule... Ni vikosi vya Nigeria chini ya mwavuli wa ECOMOG, ni umoja wa mataifa ya Afrika Magharibi… Ecomog walikuwa na jeshi lilioongozwa na k**anda kutoka Nigeria... Jeshi hilo lilifika Monrovia na meli kubwa ya kijeshi…
Jumapili Septemba 9, 1990, Rais Samuel Doe aliposikia habari za ujio wa ECOMOG, akafanya kosa kubwa la kuamua kutoka Ikulu na kwenda mwenyewe bandarini kuonana na k**anda wa vikosi hivyo vya majeshi ya Nigeria... Samuel Doe hakuwa na msafara mkubwa... Aliwachukua walinzi wake na kuingia kwenye Mercedes Benz kuelekea bandarini…
Masikini, Rais wa nchi akajikuta anapita kwenye mji wenye miba… Akafika bandarini na hapo Prince Johnson alikuwa amewapanga askari wake kumshughulikia Samuel Doe… Zikapigwa risasi na walinzi wote wa Samuel Doe wakapoteza maisha… Samuel Doe mwenyewe risasi ilimpata mguuni na hakuweza kukimbia, akak**atwa…
Akafungwa kitambaa usoni na akapelekwa kwenye kuteswa... Prince Johnson akahakikisha mateso yale yanarekodiwa kwa kamera za filamu... Kwenye filamu hiyo, Prince Johnson anaonekana akipungiwa upepo na mwanadada huku akinywa bia na kumwangalia rafiki yake wa zamani, Samuel Doe akiteswa… Muda mwingi Prince Johnson alikuwa akimtaka Samuel Doe aseme zilipo fedha kwenye hazina…
Kuna wakati alisikika Samuel Doe akimwita rafiki yake wa zamani kwa jina alilozoea kumwita: "Prince, waambie walegeze kamba walizonifunga, nitasema kila kitu, walegeze hizo kamba kwanza!"…
Ukweli, kamba walizomfunga kwenye miguu na mikono zilikaza sana na kumletea maumivu makali… Waliendelea kumpiga huku wakimtaka ataje ilipo hazina. Walimtaka ataje akaunti yake ya benki…
Ndivyo ilivyokuwa barani kwetu Afrika, na labda mpaka leo… Rais dikteta anapopinduliwa, kikubwa kinachotafutwa ni namba ya akaunti ya benki alikoficha fedha… Mara nyingi ni kwenye benki za nje… Ndio, inahusu hazina ya nchi…
"Mkateni sikio k**a hataki kusema!" Alisikika Prince Johnson akitamka kwa hasira…
Askari wale wakamtupa Samuel Doe sakafuni, wakamkata sikio moja…
"Mkateni sikio lingine!", alisikika tena Prince Johnson akitamka…
Baada ya hapo, Rais Doe aliuawa kikatili Jumapili hiyo jioni, Septemba 9, 1990 baada ya kukatwa masikio yake, sehemu zake za siri na baadhi ya vidole vya miguu na mikono na hatimae mwili wake ulitembezwa mitaa mbalimbali ya jiji la Monrovia…
Huo ndio ulikuwa mwisho wa Dikteta Samuel Kanyon Doe wa Liberia.

06/05/2021

IJUE "APP" BORA YA SIMU KWA WANANDOA KULIKO ZOTE.

✍️

INAITWA 👇
"Period Tracker Flo, Pregnancy & Ovulation Calendar"

Hii ni programu ambayo mara nyingi hutumiwa na wanawake au wanaume ambao wapo katika mahusiano ili kupata taarifa sahihi kuhusu mzunguko wa hedhi wa wapenzi wao. Kwa mara ya kwanza utakapo ifungua programu hii utatakiwa kuweka tarehe ya hedhi.

Pia inakupa maelezo kuhusu uwezekano wa kupata ujauzito. Kwa hiyo mbali na taarifa za hedhi, pia ni programu nzuri k**a unahitaji kupata mtoto, itakujulisha siku ambayo kuna *uwezekano mkubwa wa kupata mtoto, na itakwambia jinsia ya mtoto, tabia, na vingine vingi ikitegemea vile ulivoweka taarifa zako.*



NI MABINGWA WA VIFAA VYOTE VYA UMEME

| *WINDOWS ZOTE ZIPO*


N.k

0766199564 / 0622986231
IRINGA TOWN


#(ICT)2021

02/05/2021

WAFAHAMU "VIRUS" 10 WA COMPUTER WALIOTISHA DUNIANI.

(KUNA VIRUS MOJA ILIITWA "I LOVE YOU" ILI KUSHAWISHI WATU KUBOFYA.

✍️

*1.Code Red*

Kirusi cha Code Red kiliibuka mnamo mwaka 2001 na kubainiwa na wafanyakazi wawili wa eEye Digital Security. Kirusi hiki kiliitwa Code Red kwa sababu wafanyakazi hao walikuwa wanakunywa “Code Red Mountain Dew” wakati walipokibaini.

Kirusi hiki kilipoibuka kililenga seva za Microsoft IIS, na kilijizalisha kwa kiasi kikubwa ili kuteka mfumo mzima wa kompyuta. Kirusi hiki kilisambaa kwa kasi hadi kufanikiwa kuathiri seva za ikulu ya Marekani.

Ndani ya muda usiozidi wiki moja, kirusi hiki kilikuwa kimeshazima seva 400,000 na kompyuta milioni moja duniani kote. Inakadiriwa kuwa kirusi hiki kilisababisha hasara ya takriban dola milioni 2.6 za Marekani.

*2. CryptoLocker*

Hiki ni kirusi kilichokuwa kinaathiri kompyuta za Window, kirusi hiki kilificha mafaili ya mtumiaji na kumtaka alipe kikombozi (Ransom) ili apate tena mafaili yake.

Virusi vya aina hii bado vinaendelea kutumiwa na kutengenezwa na wadukuzi duniani. Virusi hivi hudai malipo ya fedha ili kufungua tena mafaili ya mtumiaji; ikiwa hatalipa pesa hizo kwa wakati atapoteza mafaili yake daima.

*3. MyDoom*

Hiki ni kirusi kilichoibuka manamo mwaka 2004 na kuathiri kompyuta zilizokuwa zinatumia programu endeshi ya Window; kirusi hiki kilikuwa kikisambaa kwa kasi sana kwa njia ya barua pepe baada ya kile cha ILOVEYOU.

Inaaminika kuwa kirusi hiki kilitengenezwa na mtu aliyelipwa kwani kilikuwa na maandishi “Andy; I’m just doing my job, nothing personal, sorry,” – (Andy; Ninafanya kazi yangu, hakuna kitu binafsi, samahani)

Inakadiriwa kirusi hiki kilisababisha hasara ya takriban dola bilioni 38.

*4. Melissa*

Kirusi cha Melissa kilitengenezwa na David L. Smith mwaka 1999. Kirusi hiki kilianza kusambaa kupitia faili la Microsoft word lililokuwa linadaiwa kuwa na nywila (password) za tovuti za ngono. Inadaiwa kuwa mtumiaji alipopakua faili hili na kulifungua ndipo kirusi hiki kilipoingia kwenye kompyuta yake.

Kirusi hiki kilituma barua pepe kwenda kwenye orodha ya watu wote walioko kwenye barua pepe ya mwathirika ili kujisambaza. Kirusi hiki kiliathiri taasisi za kiserikali, benki na hata watu binafsi.

Taasisi mbalimbali za kiusalama zilifanikiwa kumk**ata David L. Smith ndani ya kipindi kisichozidi wiki moja tangu kutengenezwa kwa kirusi hiki. Inakadiriwa kuwa kilisababisha hasara ya dola milioni 80.

*5. Sasser*

Kirusi hiki kiliibuka mnamo mwaka 2004, na kilibuniwa na mwanafunzi wa sayansi ya Kompyuta Sven Jaschan aliyebuni pia kirusi cha Netsky.

Kirusi hiki kiliathiri mfumo wa uwakaji wa kompyuta na kuifanya izime mara kwa mara. Kirusi hiki pia kilijizalisha na kujisambaza kwa kasi kupitia mtandao; inakadiriwa kuwa kilisababisha hasara ya dola bilioni 18.

*6. Stuxnet*

Inaaminika kuwa kirusi hiki kilitengenezwa na jeshi la Israeli kwa kushirikiana na Marekani, Stuxnet ni mfano wa silaha ya kivita ya kompyuta (Cyberwarfare).

Kirusi hiki kililenga kuathiri mfumo wa kompyuta wa viwandani (Programmable Logic Controller – PLC) wa vinu vya nyukilia vya Iran.

Inadaiwa kuwa kirusi hiki kililenga kuharibu mfumo wa vinu hivyo na kuvifanya viongeze kasi ya utendaji na hatimaye kulipuka. Mfumo uliolengwa ni ule uliotengenezwa na Siemens; hata hivyo baadae Siemens walikabili kirusi hiki.

*7. Conficker*

Kirusi hiki kinafahamika pia k**a Downup au Downadup, kilibainika mnamo mwaka 2008. Kirusi hiki kiliathiri kompyuta kwa njia ya kuifanya iwe botnet. Botnet ni watumiaji bandia wanaotengenezwa ili kufanya uvamizi wa DDoS.

Uvamizi wa DDoS ni udukuzi unaohusisha kuzalisha maelfu au mamilioni ya watumiaji bandia wanaotembelea tovuti fulani kwa wakati mmoja; hili huifanya tovuti husika ishindwe kuwahudumia wote na kusababisha tovuti hiyo isipatikane.

Inakadiriwa kirusi cha conficker kilisababisha hasara ya takriban dola bilioni 9.

*8. Zeus*

Kirusi hiki kililenga kufanya matendo mbalimbali ya kihalifu kwenye tarakilishi ya mhanga. Kirusi cha Zesus kiliiba taarifa za siri na kumdanganya mtumiaji kufanya mambo mbalimbali ambayo kiuhalisia yangeweka usalama wake hatarini zaidi.

*9. Flashback*

Kirusi hiki kilichoibuka mnamo mwaka 2011, hakikuwa maarufu sana lakini kilidhihirisha udhaifu kwenye kompyuta za Mac. Kirusi hiki kilimdanganya mtumiaji kusakinisha (install) programu ya Flash, kisha kuivamia kompyuta yake na kuifanya kuwa *botnet.*

*10. ILOVEYOU*

Hiki ni kirusi cha kompyuta kinachoaminika kusababisha athari kubwa sana duniani. Kirusi hiki kilibainika mnamo mwaka 2000 na kuanza kusambaa kwa kasi kubwa kupitia barua pepe.

Inakadiriwa kuwa kirusi hiki kilisababisha athari ya dola zaidi ya bilioni 15, pia inaaminika kuwa asilimia 10 ya kompyuta zote zilizokuwa zimeunganishwa kwenye mtandao duniani ziliathirika.

Kutokana na athari za kirusi hiki, mashirika na taasisi mbalimbali zikiwemo za kiserikali zilizima kompyuta zake ili kukabiliana na kirusi hiki.

KARIBU IRINGA TOWN UKUTANE NA "MlewaElectronics".


+WINDOWS MPYA KUFANYA computer yako kuwa nyepesi.



N.k

0766199564 / 0622986231

(I.C.T)

27/04/2021

FAHAMU HII KUHUSU "PATTERN" ZA SIMU.



Katika uchunguzi uliofanywa na aliyekuwa mwanafunzi wa chuo cha *Norwegian University of Science and Technology,* "Marte Løge", alibaini kuwa kati ya ‘pattern’ 4000 asilimia 77 walikuwa wanaanza kuchora kuanzia katika moja kati ya kona nne za juu kabisa. Asilimia 40 walianza katika kona ya juu upande wa kushoto kabisa.

Kwa haraka haraka watu wengi huwa wanaanza kuchora *‘pattern’* zao na kwa kupitia katika vinundu vinne tuu mpaka vitano saa zingine. Kwa kufanya hivyo wanashusha ule ugumu wa kuweza kutoa loki hizo. Sawa kwa mtu kukisia bado ni vigumu lakini kwa watu ambao wamebobea kwenye TEHAMA k**a *"Mlewa"* wanaweza wakawa wamerahisishiwa kazi ya kudukua au kufanya chochote kwa kiasi flani.

Katika ‘Pattern’ kuweka shepu za herufi k**a vile “L” au “Z” kuanzia katika kona ya kushoto ya juu ni rahisi sana kwa mtu kuotea kwani zinajulikana sana. Pia watu wanafeli pale wanapoweka herufi hizo kutoka kwa majina yao au kutoka kwa watu wao wa karibu.

Nadhani tunakubaliana kuwa k**a unatumia aina hizo za *‘Pattern’* ni rahisi sana mtu kuiotea na akafanikiwa kutoa loki katika kifaa chako.

Sasa ni njia gani za kufanya kuhakikisha kuwa unakuwa na *‘Pattern’* ambayo sio rahisi kwa mtu kuiotea?. ```USISITE! NITAFUTE TUZUNGUMZE MENGI KUHUSU TEHAMA (I.C.T)
0766199564 / 0622986231

Computer


& Vifaa Vyote Vya Umeme

IRINGA TOWN
MWEMBETOGWA.

17/04/2021

LIJUE BALAA LA MGUNDUZI WA FACEBOOK"

________________

** ✍️

⬛...SHILINGI *MILIONI 45.8,* SAWA NA ($20.000) NDIZO ZINAZOTUMIKA KILA BAADA YA SIKU MOJA KWA AJIRI YA KUMLINDA MWANZILISHI WA MTANDAO WA *"FACEBOOK"* (MARK ZUCKERBERG), NA INATAJWA BAJETI YA TSh *BILIONI 16.7* ZIMETENGWA KWA AJIRI YA KUMLINDA "MARK" NA FAMILIA YAKE KWA MWAKA MMOJA.* 👇

⬛... ```PIA FAHAMU KWAMBA...."FACEBOOK" IMETAWALIWA NA RANGI YA "BLUE" KWA SABABU TU YA MWANZILISHI WAKE HUYU ANA TATIZO LA KUSHINDWA KUTOFAUTISHA RANGI "NYEKUNDU" & "KIJANI" NA KWAKE RANGI YA "BLUE" TU NDIYO ANAYOIONA VIZURI KULIKO RANGI ZOTE DUNIANI.```

KARIBU TUSHAULIANE KUHUSU "I.C.T"...(IRINGA MJINI)

0766199564 / 0622986231

16/04/2021

Je! COMPUTER YAKO IPO "SLOW"? FANYA HIVI ILI IWE NA KASI "IWE FASTA"

✍️

*1. Weka Anti Virus.*

"NB: Virusi vya kompyuta vitatumia sehemu kubwa ya RAM na HDD katika kutekeleza majukumu yake.

*2. Futa Temporary Files*

Kwa watumiaji wa Windows unaweza ukafungua my computer=>Nenda local disk C: au disk yenye Windows=> Fungua Users => Chagua User k**a jina la mtumiaji lipo => AppData=> Local=>Temp

Hapo unaweza ukafuta mafaili yote yaliyomo kwenye hilo folder la temp, kisha restart kompyuta yako.

*3. Punguza vitu katika Hard Drive yako*

*4. RAM ya kompyuta yako ni ndogo, ongeza RAM*

📌Windows XP kiasi kidogo cha RAM kiwe 1GB

📌Windows 7 kiasi kidogo cha RAM kiwe 2GB

📌Windows 8, 8.1 na 10 kiasi kidogo cha RAM kiwe 4GB

*5. Funga baadhi ya Programs k**a unarun Programs nyingi kwa pamoja*

*6. Update Windows yako (Mfumo endeshi)*

Ni muhimu sana kuupdate windows yako kila updates zinapotoka sababu updates zinakuja na maboresho mengi hasa ya kuisalama katika kompyuta yako.

*7. Punguza Add-Ons kwenye browser (kivinjari) yako*

Wingi wa Add-on kam vile youtube downloader, ruler, games, znet hupunguza ufanisi wa kompyuta kwa kiasi kikubwa sana, hivyo hakikisha unaunistall baadhi ya add-on ambazo huzitumii mara kwa mara.

KUTANA NA "Mr: MLEWA" MTAALAMU WA TEHAMA (ICT), IRINGA TOWN.

0766199564 / 0622986231


#(I.C.T)

25/03/2021

UTATA JUU YA KIFO CHA RAIS "JF KENNEDY" WA MAREKANI

✍️
...Risasi hii ilipigwa katika muda ambao Rais Kennedy, mkewe Jackie na Gavana Connally wote walikuwa wamegeukia mkono wa kushoto kupungia wananchi na ghafla wote wakageuka mkono wa kulia kupungia wananchi walio upande huo.

Ni muhimu kukumbuka kwamba katika muda huu walikuwa wekwisha lipita Jengo la *Texas School Book depository,* na wamelipa mgongo kwa kuliacha umbali wa takribani mita 81.

Risasi ya pili kupigwa (risasi ya kwanza nitaiongelea baadae) ilifyatuliwa sekunde ambayo Rais *Kennedy* ameinua mkono mmoja juu akiwapungia wananchi.

Risasi hii ilimpenya nyuma yake katikati kabisa ya shingo na nyama ya juu ya bega na kusababisha uharibu Mdogo kwenye uti wa mgongo, na kisha kupenya ndani na kuharibu sehemu ya juu kabisa ya pafu la kulia na kutokea kooni ikiharibu sehemu kubwa ya koromeo.

Baada ya kupigwa na risasi hii, katika kipande cha video unaweza kumuona Rais Kennedy akiwa amekunja ngumi na kuelekeza mkono mbele ya uso wake usawa wa mdomo k**a vile anakohoa na kuinama kwa mbele kidogo akiegemea upande wa kushoto aliko mkewe.

Pia unaweza kumuona mkewe akiwa anamkumbatia kwa kuzungusha mkono wake mabegani kwa Kennedy kumuuliza k**a yuko 'OK'! (Mpaka muda huo hakujua k**a mumewe amepigwa risasi).

Risasi hii hii ya pili iliyompiga Kennedy, ilipotoka kooni kwa Kennedy ilienda moja kwa moja ya kumpiga Gavana Connally!
Risasi hii ilimpiga Gavana Connally mgongoni chini kidogo ya kwapa upande wa kulia na kutengeneza tundu la umbo la duara na kuharibu kiasi cha inch 4 cha mbavu yake ya tano upande wa kulia na kisha kutokea kifuani katika chuchu.

Risasi hii hii baada ya kutoka kifuani kwa Gavana Connally kupitia kwenye chuchu ilitua kwenye mkono wa kulia wa Gavana Connally, juu kidogo ya kiganja na kuvunja vunja sehemu hiyo katika vipande vinane.

Risasi hii hii, hatimaye ikatua kwenye paja la kushoto la Gavana Connally.

(Nitaeleza huko mbeleni kuhusu utata wa risasi hii ya pili iliyompata Kennedy na Gavana Connally kwa pamoja na ile Risasi ya kwanza ambayo haikuleta madhara yoyote).

Risasi ya pili kumpata rais (ambayo ilikuwa ni risasi ya tatu kupigwa) ilimpata kichwani upande wa juu kulia.

Risasi hii ilifumua kabisa eneo hilo la kichwa na kusababisha sehemu ya ubongo wa mbele kumwagika.

Damu nyingine ikaruka nyuma ya gari kwenye 'trunk' na nyingine kutua mpaka kwenye mkono wa kushoto wa afisa wa *Secret Services* aliyekuwa anaendesha gari ya wanausalama waliokuwa gari ya nyuma ya Rais.

Ndani ya sekunde mbili baada ya mumewe kufumuliwa na risasi kichwani, First Lady Jacqueline Kennedy akaruka kutoka kwenye siti yake na kuanza kuparamia nyuma ya gari kwenye trunk.

Tofauti na wengi wanavyodhani kwamba alikuwa anajaribu kukimbia kuokoa maisha yake, ila ukweli ni kwamba alikuwa anaokota kipande cha mfupa wa fuvu la kichwa kilichodondoka kwenye nyuma ya gari kwenye trunk baada ya mumewe kufumuliwa kichwa na risasi. Baada ya kukichukua haraka haraka akarejea kwenye siti yake. (Tafuta kipande cha video na ujoridhishe zaidi).

Sekunde hii hii ambayo First Lady alikuwa anaparamia gari kwenye trunk, katika gari ya nyuma (follow up car), Special Agent Clint Hill ambaye alikuwa ananing'inia kwenye mlango wa mbele kushoto akaruka na kuanza kuikimbilia gari iliyombeba rais na first lady.
Dereva wa gari la rais alikuwa ameongeza mwendo baada ya mushkeli kutokea na dhahiri kuonekana kwamba rais yuko hatarini.
Hivyo basi ilimbidi Clint Hill kujaribu kuparamia gari mara kadhaa mpaka alipofanikiwa kuidandia gari na mara moja kuwafunika rais na first lady akiwakinga kwa kutukia mwili wake k**a ngao.

Baada ya Agent Clint Hill kuwakinga Rais na mkewe dhidi ya shambulio lingine lolote la risasi kuwafikia, gari ya rais liliendeshwa kwa kasi kubwa likifuatiwa na pikipiki za pembeni na ile follow up car ya maafisa usalama.

Wakati haya yote yanatokea zilikuwa zimebaki takribani dakika tano pekee kufika walikokuwa wanaelekea, *Trade Mart.*
Kwahiyo baada ya gari iliyombeba rais kuanza kuendeshwa kwa kasi, takribani saa 6 na dakika 35 walipita eneo la Trade Mart na kuelekea moja kwa moja hospitali ya Parkland Memorial Hospital ambako waliwasili majira ya saa 6 na dakika 38 na kupokelewa kisha *Rais Kennedy* alipelekwa moja kwa moja chumba cha dharura.

Licha ya watu wa usalama kujitahidi sana kuratibu taaarifa za kilichotokea zisivuje kabla ya taarifa rasmi ya serikali, lakini majira ya saa 6 na dakika 40 kituo cha televisheni cha CBS kikakatisha Igizo lililokuwa linaonyeshwa kwenye televisheni yao na kutoa *"Breaking News" kuwa msafara wa Rais WETU KIPENZI umeshambuliwa huko Dallas.*

Baadae k**a muda wa saa 6 na dakika 45, Dan Rather mwandishi wa habari wa kituo cha CBS alifanya mawasiliano kwa siri sana na daktari anayemfahamu hapo hospitalini na kuvujishiwa taarifa kuwa kuna uwezekano mkubwa Rais Kennedy hayuko hai.

Ifahamike kwamba maafisa wa Secret Services waliwaleta hapa viongozi wengine wote wakuu waliopo kwenye msafara, yaani First Lady Jacqueline Kennedy, Makamu wa Rais Johnson, Mkewe Lady Bird na Gavana Connally ambaye alikuwa chumba cha wagonjwa mahututi.

Ilipofika saa 7 kamili madaktari wakatoa taarifa yao kwa viongozi wa serikali na wanausalama waliokuwepo hapo kwamba, licha ya kutumia ujuzi wao wote na maarifa yao yote, *wameshindwa kuokoa maisha ya Rais JF Kennedy, kwamba Rais Kennedy amefariki.!!*

Huko mtaani habari zilikuwa zinaenea kwa kasi k**a moto wa kifuu, kuwa Rais Kennedy amefariki, hivyo kwa busara watu wa usalama wakashauri kuwa itolewe taarifa rasmi kuhusu kifo cha Rais Kennedy ili kuepusha mkanganyiko na taharuki iliyopo mtaani.

Makamu wa Rais Johnson akakubali hilo lakini akaamuru taarifa hiyo itolewe kwa umma mara baada ya yeye kuondoka hapo hospitali kwa sababu ya usalama wake, kwamba hataki yeyote ajue kuwa yuko hapo hospitali kwa kuwa kwa vile Rais ameuwawa tayari yawezekana yeye k**a Makamu wa Rais akawa ni "next target"!

Saa 7 na dakika 26 Makamu wa Rais Lyndon B. Johnson akaondolewa kwa siri kubwa kutoka Parkland Memorial Hospital na kupelekwa uwanja wa ndege wa Love Field ambako Airforce One ilikuwa imepaki.

Baada ya Makamu wa Rais kuondoka tu, dakika saba baadae yaani saa 7 na dakika 33 Katibu Msaidizi wa Mawasiliano Ikulu Bw. Malcolm Kilduff ya Marekani akafanya mkutano na waandishi wa habari hapo hapo hospitali na *kuutangazia rasmi ulimwengu kuwa Rais JF Kennedy amefariki baada ya kudunguliwa na risasi na mtu asiyejulikana.*

Bw. Kilduff hakujibu swali lolote la waandishi wala kutoa taarifa nyingine yoyote. Alipotoa taarifa hii tu akaumaliza mkutano na wanahabari.

Baada ya waandishi wote kuondoka na kubakia watu wa serikali pekee na wanausalama ndani ya Hospitali kulitokea kisa ambacho naamini wengi hawajawahi kukisikia.

Ni kwamba, katika sheria za Marekani kipindi hicho zilikuwa zinaelekeza kwamba, endapo Rais atafariki akiwa jimbo Fulani.. Mwili wake unakuwa chini ya mamlaka ya jimbo na sio serikali kuu.

Sasa, yule bwana swahiba wa Rais Kennedy na Katibu wake wa teuzi Kenneth O'Donnell, yule ambaye alimuamuru Afisa wa Secret Services, Agent Kellerman kuwa gari la Rais liondolewe paa na kubaki 'kibnda wazi', akatoa tena maelekezo kwa wanausalama wauondoe mwili wa Rais Kennedy kutoka hapo hospitalini na kuipeleka uwanja wa ndege wa Love Field na kuipakia katika Air Force One.

Lakini madaktari walikataa mwili huo kuondolewa hospitalini bila kufanyiwa 'Autopsy' (uchunguzi wa kina wa kidaktari kuhusu chanzo cha kifo) ukizingatia kuwa Rais Kennedy amekufa kwa mauaji ya kukusudiwa.

Bw. Kenneth O'Donnell akasisitiza kuwa hakuna muda wa kutosha kufanya Autopsy kwani Air Force One inatakiwa iondoke mara moja kuwarudisha Makamu wa Rais na First Lady Washington kwa sababu za kiusalama na First Lady amekataa kuondoka bila mwili wa mumewe....INAENDELEA.


*NB.* HAJAWAHI TOKEA RAIS WA MAREKANI ALIYEPENDWA NA RAIA WAKE KUMZIDI HUYU "JF KENNEDY" ALIONGOZA NCHI KWA MIAKA MIWILI NA NUSU TUU!!! MWAKA WA *(1961-1963)*

KUTANA NA "MlewaElectronics" MAGWIJI WA...*👇

📌 *COMPUTER*
📌 *Tv*
📌 *SIMU*
📌 *RADIO & Vifaa Vyote Vya Umeme

#0766199564 / 0622986231
IRINGA TOWN | JIRANI NA UWANJA WA MWEMBETOGWA

#(I.C.T)

Want your school to be the top-listed School/college in Iringa?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Iringa