Mwl Elisha Mathayo

Mwl Elisha Mathayo

Share

Teaching Word of God

06/01/2026

KUMFUATA KRISTO KATIKA UTUMISHI

Bwana Yesu asifiwe watumishi wa Mungu mnaendeleaje? Heri ya mwaka mpya 2026

Leo natamani tushirikishane Neno moja muhimu sana linalohusu utumishi wetu kwa Mungu (Kumtumia Mungu)

Neno la kusimamia ni kutoka katika injili ya Yohana 12:26

[26]Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.
If any man serve me, let him follow me; and where I am, there shall also my servant be: if any man serve me, him will my Father honour.

Katika mstari huo Yesu anafundisha kitu muhimu sana kinachohusu utumishi wetu kwake kwanza anasema
akinitumikia na anifuate ... Hapa tunaelewa kwamba kumtumikia Mungu ni kumfuata Yeye kumfuata Kuna maana mbili
a) Maana ya kwanza ni Kumwamini awe Bwana na Mwokozi wa maisha Yako (Kuwa mfuasi wake)
b) Maana ya pili Ni kufuata maelekezo yake yaani kumsikiliza ....

Hapa tunajifunza kwanza mtu yeyote atakayesema anamtumikia Mungu lazima kwanza awe mfuasi wa Yesu yaani lazima Yesu awe Bwana na Mwokozi wake kikwelikweli lakini pia tunaona kuwa hakuna namna tunaweza kumtumikia Mungu k**a Hatufuati maelekezo yake hatufuati anachosema

1 Wakorintho 11:1
[1]Mnifuate mimi k**a mimi ninavyomfuata Kristo.
Be ye followers of me, even as I also am of Christ.

Mojawapo ya sababu ya Mtume Paul kufanikiwa katika huduma yake ni aliamua kumfuata Kristo( Kumsikiliza na kumwamini Kristo) ... HAKUNA KUFANIKIWA KWENYE HUDUMA BILA KUMFUATA KRISTO

KWA NINI NI LAZIMA/ MUHIMU KUMFUATA KRISTO KATIKA UTUMISHI?
1: Kazi sio yetu ni yake..Hii inatufanya tumfuate kwa kila kitu kwa sababu sisi sio wenye malengo na sisi sio wenye maono na kazi hiyo na kimsingi hata faida sio Yetu ni yake kwa hiyo k**a tunataka kumtumikia Mungu lazima tumsikilize kwa kila kitu

2;Yeye ndiye anaejua namna ya kuifanya kazi na ikaleta matokeo anayoyataka Yeye ....Ukweli ni kwamba Sisi tunaweza tukawa tunahisi tu au tuna uzoefu tu kwa namna ya kawaida ila kimsingi Mungu ndiye anaejua namna kazi inavyofanyika kila hatua ili ilete matokeo kwa hiyo lazima tumfuate na kumsikiliza yeye tu

3:Yeye ndiye atakayetulipa baada ya kazi..... Ukisoma huo mstari pale mbele unasema mtu akinitumikia baba atamuheshimu... Kwa lugha nyepesi Mungu atamlipa sasa Mungu hawezi kutulipa k**a tulifanya kwa mawazo na fikra zetu tu lazima tufanye k**a anavyotaka yeye ndipo atakapotulipa sawasawa na kazi yetu....

FAIDA ZA KUMFUATA KRISTO KATIKA UTUMISHI
1:Ukimfuata Kristo utafanya kazi ambayo
Mungu anataka ifanyike
2:Utafanyia kazi mahali ambapo Mungu
anafanyia
3: Utafanya kazi ya Mungu kwa wakati
ambao Mungu anataka ufanye (wakati
uliokubalika

Ndugu zangu, watumishi wenzangu ukitaka kazi yoyote au huduma yoyote unayoifanya ifanikiwe msikilize Mungu na mfuate Mungu Fuata anachosema hata k**a ni kigumu fanya tu hata k**a haujaelewa wewe fanya tu hata k**a unahisi tofauti wewe fanya kile Mungu amesema ... Utamuona Mungu kwa namna ya ajabu sana...

Nakutakia mwaka mwema uliojaa utumishi kwa uaminifu mkubwa mbele za Mungu Na Neema ya Mungu wetu mwema ikuhifadhi na kukutunza kwa jina l a Yesu ..

Ndimi rafiki yako
Mwl Elisha Mathayo
0713133123

01/01/2026

Shetani ni adui lazima apingwe kwa jina la Yesu

Photos from Mwl Elisha Mathayo's post 27/07/2025

Utukufu kwa Mungu kwa ajili ya ibada ya leo hakika tumemuona Mungu akituhudumia kwa namna ya ajabu sana

SUNDAY SERVICE
Phm Mtwivila - The City of Refuge Church
27- July- 2025



📸By IT BENCH

02/09/2024

KANUNI YA KUOMBA
Kwa nini lazima tuombe kwenye kila jambo?
1 Thessalonians 5:17
Pray without ceasing. (ombeni bila kukoma)

Maisha tunayoishi hapa duniani ni maisha ya kanuni kila wakati tunapotaka kufanikisha jambo fulani lazima tujikite katika kanuni zake
Katika nyakati hizi za mwisho watu wengi hutaka mambo yatokee bila kufuata kanuni ndio maana kuna wakristo wengi wasio na matokeo kwa sababu hawataki kufuata kanuni za utokeaji wa matokeo

Jambo moja la kufahamu ni kwamba hakuna jambo lisilo na kanuni na Mungu ni Mungu wa kanuni na anaishi na kufanya mambo yake kwa kanuni , kuna mambo mengi ambayo watu wanashindwa kuyafikia kwa sababu hawajaamua kuzifuata kanuni

Kwa nini kila jambo lina kanuni yake?
Kila kitu unachokiona kwa macho ya damu na nyama kina chanzo chake ambacho hakionekani (katika Ulimwengu wa Roho)
Ngoja niseme kidogo kuhusu Ulimwengu wa Roho
Ulimwengu wa Roho ni ulimwengu usioonekana kwa macho ya damu na nyama ila ndio ulimwengu unaoongoza huu unaonekana kwa macho ya damu na nyama kwa sababu vinavyoonekana vyote si vya kudumu na ni matokeo ya vile visivyoonekana
Ulimwengu wa roho una nguvu kuliko huu wa macho ya damu na nyama kila jambo linalotokea hapa duniani huwa limeshatokea katika Ulimwengu wa Roho. Ulimwengu wa roho hauna bahati mbaya wala hauna bahati kila kitu kinaendeshwa kwa kanuni na ni ulimwengu usio tania ulimwengu ambao viumbe wake wako serious na kazi zao kuliko huku duniani.

Ulimwengu wa Roho umetawaliwa na Viumbe wa rohoni ambao ni roho, viumbe hawa wamegawanyika katika maeneo mawili
1: Viumbe wa roho wa Nuru ( Upande wa Mungu)
2: Viumbe wa roho wa Giza ( Upande wa Shetani)

25/12/2023

Mathew 1:21

Photos from Mwl Elisha Mathayo's post 03/12/2023

Tunamtukuza Sana Mungu wetu kwa ajili ya jumapili ya leo ..
Tumekuwa na wakati mzuri sana wa ibada ya sikukuu ya vijana CFD's hakika tumemuona Mungu



📸 by IT BENCH

22/06/2023

Kanisa lazima lifundishe watoto kumpenda Mungu

22/06/2023
Photos from Mwl Elisha Mathayo's post 14/06/2023

ˡᵒᵛᵉ ʷⁱˡˡ ᵃˡʷᵃʸˢ ʷⁱⁿ❤

Want your school to be the top-listed School/college in Iringa?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Iringa
Iringa