Mr Meshacking

Mr Meshacking

Share

MUNGU NI MWEMA
(GOD IS GOOD)

15/06/2026

GHOST OF TANVERI
SEHEMU YA KWANZA (01)
***

Mvua kubwa ilikuwa ikinyesha nje ya kuta kubwa za Black Dome Prison. Radi zilikuwa zikilimulika anga lililo tawaliwa na wingu zito lililotanda usiku huu huku ngurumo nzito zikisikika kwa sauti za mtetemo wa kuogofya ndani ya gereza hilo lenye sifa mbaya kuliko magereza yote nchini Tanveria.

Kwenye jengo namba saba la wafungwa hatari, wanaume zaidi ya mia mbili walikuwa wamesimama kwenye foleni ndefu wakisubiri kupata chakula cha usiku. Askari waliokuwa juu ya mnara wa ulinzi walizungusha taa kali huku bunduki zao zikiwa tayari kwa matumizi muda wowote.

Kelele za wafungwa, na matusi ya hapa na pale vilisikika kwa wingi eneo hilo.

Mwanaume mmoja mwenye mwili mwembamba, macho yake yakiwa ni myekundu, na kovu kubwa shingoni alikuwa amesimama nyuma ya mfungwa mpya aliyekuwa kimya muda wote kwenye foleni hiyo ya chakula.

“Oya… wewe ni mgeni, sio?” mwanaume huyo alihoji kwa sauti ya chini, lakini mfungwa huyo mpya hakujibu chochote.

“Unaonekana mlaini sana, sijui umefikaje hapa,” mwanaume huyo aliendelea kuongea lakini bado hakupata jibu lolote. Alitabasamu kwa dharau na kuongeza,

“Sikiliza brother… hili sio gereza la watu wa aina yako. Humu wamejaa wauaji hatari na magaidi. Sidhani k**a na wewe upo kwenye kundi lolote la watu hawa niliowataja.”
Mfungwa huyo mpya aliendelea kusimama kimya huku macho yake akiwa ameyakaza mbele, kwenye beseni kubwa la chakula.

“Humu ndani kufa ni jambo la muda mfupi sana. Sidhani k**a wewe utaweza kudumu humu.”
Safari hii, mfungwa mpya aligeuza macho yake taratibu na kumtazama jamaa huyo aliyekuwa anaongea bila mpangilio.

“Ni heri ukashughulika na mambo yako, huenda ukayanusuru maisha yako,” mfungwa mpya aliongea kwa msisitizo huku akimkazia macho jamaa huyo.

“Sura yako na maneno yako haviendani kabisa, hivi unadhani unanitisha" Jamaa huyo anaongea kwa msisitizo lakini mfungwa huyu mgeni aliishia kumuangalia tu pasi na kusema lolote

"Ila kwa kuwa umechagua kuwa mkaidi, wacha tuone itakavyokuwa,” jamaa alipiga mkwara, lakini mfungwa huyu mpya hakuonekana kuwa hata na chembe ya uoga.

Foleni iliposogea mbele, alichukua trei yake ya chakula yenye ugali na maharage yaliyochemshwa. Akageuka na kuanza kuondoka zake, akimuacha huyu jamaa akimshangaa huku akiwa na maswali mengi kichwani.

*****

Usiku huo huo wa mvua kubwa, pembezoni mwa jiji ndani ya jumba kubwa la kifahari lililozungukwa na walinzi wenye silaha nzito, magari ya thamani yalikuwa yameegeshwa nje huku kamera za usalama zikiwa zimejaa kwenye jengo hilo.

Ndani ya chumba kikubwa chenye mwanga hafifu, watu watatu walikuwa wamekaa kwenye sofa za thamani wakinywa mvinyo wa gharama kubwa.

Mwanamama mmoja mwenye ngozi ya kahawia iliyong’aa, aliyevalia suti nyeusi ya kifahari alikuwa amekaa kwenye sofa dogo lililopo kwenye chumba hicho, macho yake yakiwatazama kwa bashasha wanaume wawili waliokuwepo ndapi humo, ambao nao walikuwa wamevalia suti zilizowakaa vyema kwenye miili yao.

Mwanamama huyo alijulikana kwa jina la Madam Lucy.
Ndani ya serikali ya Tanveria, wengi walimfahamu k**a msaidizi maalumu wa mkurugenzi wa TISA, Madam Lucy ni moja kati ya watu wanaoogopeka sana hapa nchini Tanveria.

“Kwahiyo ni rasmi?” mmoja kati ya wanaume hao aliuliza huku akiweka glasi yake mezani.

“Mwisho wake umewadia. Hakuna anayejaribu kucheza na sisi kisha akabaki salama. Never!” Madam Lucy aliongea kwa madaha huku tabasamu pana likiutawala uso wake.

“Hakika moyo wangu sasa una amani. Adrian sio mtu wa kawaida. Tunatakiwa tujipongeze kwa kuweza kumdhibiti yule shetani aliye ndani ya mwili wa malaika,” mwanaume mwingine anaongea kwa msisitizo

“Ila ili tujihakikishie ushindi huu, tunapaswa kumuangamiza kabisa huyu mtu, maana hajawahi kutabirika.”

“Sajenti Leo, unadhani Adrian anaweza kutoroka Black Dome?”

“Madam, huyu binadamu sio mwepesi kihivyo,” alijibu Sajenti Leonardo Frederick kwa msisitizo, kisha akaendelea kuongea.

“Namjua vizuri sana Adrian. Ni bora tuchukue hatua mapema kabla mashetani yake hayajaamka. Nadhani wote tunajua kuwa hata kumpeleka huko gerezani ni kwa sababu yeye mwenyewe aliamua kuwa mpole, ila bila hivyo sidhani k**a tungeweza kukabiliana naye. Kwa hiyo, kivyovyote vile, tunatakiwa kumuangamiza Adrian akiwa huko huko gerezani.”

“Sawa Sajenti Leo, hilo swala niachie mimi. Nitahakikisha huyo panya anapotea kwenye uso wa dunia hii,” K**anda Sospeter aliongea kwa kujiamini.

“Hili jambo sasa lipo mikononi mwako, Peter,” Madam Lucy alisema huku akiwatazama wawili hao.

“Ondoa shaka, Madam. Naamini dunia iko mbioni kumsahau kabisa Adrian Dominic,” alisisitiza K**anda Sospeter, na vicheko vikatawala ndani ya chumba hicho huku wakigongeana glasi zao na kunywa mvinyo huo kwa ushindi mdogo walioupata.

ITAENDELEA...

Hakikisha kuwa una like na kufollow page hii ya Story za Jay ili kuweza kusoma story kali na za kusisimuaTHE GHOST OF TANVERIA
BY WIZZY JONES
Contact: +255 785879708

CHAPTER ONE (01)
***

Mvua kubwa ilikuwa ikinyesha nje ya kuta kubwa za Black Dome Prison. Radi zilikuwa zikilimulika anga lililo tawaliwa na wingu zito lililotanda usiku huu huku ngurumo nzito zikisikika kwa sauti za mtetemo wa kuogofya ndani ya gereza hilo lenye sifa mbaya kuliko magereza yote nchini Tanveria.

Kwenye jengo namba saba la wafungwa hatari, wanaume zaidi ya mia mbili walikuwa wamesimama kwenye foleni ndefu wakisubiri kupata chakula cha usiku. Askari waliokuwa juu ya mnara wa ulinzi walizungusha taa kali huku bunduki zao zikiwa tayari kwa matumizi muda wowote.

Kelele za wafungwa, na matusi ya hapa na pale vilisikika kwa wingi eneo hilo.

Mwanaume mmoja mwenye mwili mwembamba, macho yake yakiwa ni myekundu, na kovu kubwa shingoni alikuwa amesimama nyuma ya mfungwa mpya aliyekuwa kimya muda wote kwenye foleni hiyo ya chakula.

“Oya… wewe ni mgeni, sio?” mwanaume huyo alihoji kwa sauti ya chini, lakini mfungwa huyo mpya hakujibu chochote.

“Unaonekana mlaini sana, sijui umefikaje hapa,” mwanaume huyo aliendelea kuongea lakini bado hakupata jibu lolote. Alitabasamu kwa dharau na kuongeza,

“Sikiliza brother… hili sio gereza la watu wa aina yako. Humu wamejaa wauaji hatari na magaidi. Sidhani k**a na wewe upo kwenye kundi lolote la watu hawa niliowataja.”
Mfungwa huyo mpya aliendelea kusimama kimya huku macho yake akiwa ameyakaza mbele, kwenye beseni kubwa la chakula.

“Humu ndani kufa ni jambo la muda mfupi sana. Sidhani k**a wewe utaweza kudumu humu.”
Safari hii, mfungwa mpya aligeuza macho yake taratibu na kumtazama jamaa huyo aliyekuwa anaongea bila mpangilio.

“Ni heri ukashughulika na mambo yako, huenda ukayanusuru maisha yako,” mfungwa mpya aliongea kwa msisitizo huku akimkazia macho jamaa huyo.

“Sura yako na maneno yako haviendani kabisa, hivi unadhani unanitisha" Jamaa huyo anaongea kwa msisitizo lakini mfungwa huyu mgeni aliishia kumuangalia tu pasi na kusema lolote

"Ila kwa kuwa umechagua kuwa mkaidi, wacha tuone itakavyokuwa,” jamaa alipiga mkwara, lakini mfungwa huyu mpya hakuonekana kuwa hata na chembe ya uoga.

Foleni iliposogea mbele, alichukua trei yake ya chakula yenye ugali na maharage yaliyochemshwa. Akageuka na kuanza kuondoka zake, akimuacha huyu jamaa akimshangaa huku akiwa na maswali mengi kichwani.

*****

Usiku huo huo wa mvua kubwa, pembezoni mwa jiji ndani ya jumba kubwa la kifahari lililozungukwa na walinzi wenye silaha nzito, magari ya thamani yalikuwa yameegeshwa nje huku kamera za usalama zikiwa zimejaa kwenye jengo hilo.

Ndani ya chumba kikubwa chenye mwanga hafifu, watu watatu walikuwa wamekaa kwenye sofa za thamani wakinywa mvinyo wa gharama kubwa.

Mwanamama mmoja mwenye ngozi ya kahawia iliyong’aa, aliyevalia suti nyeusi ya kifahari alikuwa amekaa kwenye sofa dogo lililopo kwenye chumba hicho, macho yake yakiwatazama kwa bashasha wanaume wawili waliokuwepo ndapi humo, ambao nao walikuwa wamevalia suti zilizowakaa vyema kwenye miili yao.

Mwanamama huyo alijulikana kwa jina la Madam Lucy.
Ndani ya serikali ya Tanveria, wengi walimfahamu k**a msaidizi maalumu wa mkurugenzi wa TISA, Madam Lucy ni moja kati ya watu wanaoogopeka sana hapa nchini Tanveria.

“Kwahiyo ni rasmi?” mmoja kati ya wanaume hao aliuliza huku akiweka glasi yake mezani.

“Mwisho wake umewadia. Hakuna anayejaribu kucheza na sisi kisha akabaki salama. Never!” Madam Lucy aliongea kwa madaha huku tabasamu pana likiutawala uso wake.

“Hakika moyo wangu sasa una amani. Adrian sio mtu wa kawaida. Tunatakiwa tujipongeze kwa kuweza kumdhibiti yule shetani aliye ndani ya mwili wa malaika,” mwanaume mwingine anaongea kwa msisitizo

“Ila ili tujihakikishie ushindi huu, tunapaswa kumuangamiza kabisa huyu mtu, maana hajawahi kutabirika.”

“Sajenti Leo, unadhani Adrian anaweza kutoroka Black Dome?”

“Madam, huyu binadamu sio mwepesi kihivyo,” alijibu Sajenti Leonardo Frederick kwa msisitizo, kisha akaendelea kuongea.

“Namjua vizuri sana Adrian. Ni bora tuchukue hatua mapema kabla mashetani yake hayajaamka. Nadhani wote tunajua kuwa hata kumpeleka huko gerezani ni kwa sababu yeye mwenyewe aliamua kuwa mpole, ila bila hivyo sidhani k**a tungeweza kukabiliana naye. Kwa hiyo, kivyovyote vile, tunatakiwa kumuangamiza Adrian akiwa huko huko gerezani.”

“Sawa Sajenti Leo, hilo swala niachie mimi. Nitahakikisha huyo panya anapotea kwenye uso wa dunia hii,” K**anda Sospeter aliongea kwa kujiamini.

“Hili jambo sasa lipo mikononi mwako, Peter,” Madam Lucy alisema huku akiwatazama wawili hao.

“Ondoa shaka, Madam. Naamini dunia iko mbioni kumsahau kabisa Adrian Dominic,” alisisitiza K**anda Sospeter, na vicheko vikatawala ndani ya chumba hicho huku wakigongeana glasi zao na kunywa mvinyo huo kwa ushindi mdogo walioupata.

ITAENDELEA...

Hakikisha kuwa una like na kufollow page Mr Meshacking ili kuweza kusoma story kali na za kusisimua.

13/06/2026

ya kutisha iliyowaacha hoi polisi.

Huko Cambridge, Massachusetts Marekani, mwaka 1969, kulitokea tukio lililobaki kuwa moja ya mafumbo yasiyo na majibu hadi leo.

Kwenye barabara tulivu ya Brattle Street, watu walianza kumuona mtu wa ajabu mwanaume aliyekuwa amevaa suti ya kawaida nyeusi, lakini uso wake haukuonekana kabisa.

Alikuwa amevaa mask ya plasta nyeupe, iliyofunika uso mzima isipokuwa macho na mdomo.

Alikuwa akija, akinunua vitu vidogo k**a aspirini au bandeji, analipa cash, kisha anaondoka kimya kimya.

Wafanyakazi wa duka la dawa la Star Pharmacy walishangaa, lakini wakaanza kumzoea… au walidhani hivyo.

Watu wakaanza kumuita jina moja tu:
“The Plaster Man” — Mtu wa Mask ya Plasta

Lakini hofu ilianza kukua.

Maana Kila wiki alikuwa anarudi.
Mask ile ile.
Kimya kile kile.
Tabia ile ile isiyoelezeka.

Baadhi ya watu walisema alikuwa mgonjwa anayeficha uso wake.
Wengine wakasema ni mhalifu anayejificha.
Lakini kuna waliodai kitu cha kutisha zaidi kwamba hakuwa mtu wa kawaida kabisa.

Kisha mambo yakaanza kubadilika.

Februari 28, 1969, mwanamke mmoja aitwaye Ellen Grayson alidai alimwona Plaster Man akiingia kwenye nyumba ya zamani iliyotelekezwa.

Nyumba hiyo ilijulikana k**a “nyumba ya laana” pale mtaani hakuna aliyethubutu kuikaribia.

Ellen alipojaribu kusogea karibu… alisikia hatua za haraka ndani ya nyumba, Kisha kimya kikuu.

Hakuna aliyethubutu kuingia tena siku hiyo.

Machi 3, 1969, polisi walipokea taarifa ya harufu mbaya kutoka kwenye nyumba hiyo.

Walipoingia ndani, waliganda.

Ndani ya chumba kulikuwa na mwili wa mwanaume amekaa kwenye kiti, akiwa amevaa mask ya plasta ile ile.

Lakini alikuwa amekufa.

Hakuna damu. Hakuna jeraha.

Karibu naye kulikuwa na chupa ya aspirini na karatasi ndogo iliyoandikwa kwa mkono:

“I’m done.”

Uchunguzi ukaanza, lakini kila kitu kikawa kisichoeleweka:

Mask ilikuwa imetengenezwa kwa mikono, na ilimkaa uso k**a ilitengenezwa kwa ajili yake pekee

Hakuna alama za vidole zililingana na mtu yeyote

Hakukuwa na kitambulisho

Sababu ya kifo: sumu isiyojulikana

Gazeti lililopatikana karibu naye lilionyesha habari za ajali ndogo wiki moja kabla lakini hakuna uhusiano uliopatikana.

Polisi walipojaribu kumtambua, hakuna aliyejitokeza.

Picha yake ilichapishwa magazetini kimya.
Hakuna aliyejua alikuwa nani.

Baada ya miezi, alizikwa k**a:

“John Doe – Mtu Asiyejulikana”

Baada ya tukio hilo, minong’ono ilienea mtaani k**a unavyojua midomo hailali na njaa.

Alikuwa jasusi wa Vita Baridi aliyeshindwa

Alikuwa mtu mwenye ugonjwa wa akili uliomfanya ajifiche

Au alikuwa mtu aliyekimbia maisha yake mwenyewe… hadi akayamaliza kimya kimya

Nyumba hiyo ya Brattle Street ilibomolewa miaka ya 1970…
lakini watu wa Cambridge bado wanadai kwamba usiku wa giza, kivuli cha mtu mwenye mask nyeupe huonekana barabarani.

Hadithi ya The Plaster Man imebaki kuwa mojawapo ya mafumbo ya kutisha zaidi ya Marekani kisa cha mtu aliyekuja kimya… akaishi kimya… na kufa bila kujulikana.

Just a boy From chamangi.The man in plaster mask; hadithi ya kutisha iliyowaacha hoi polisi.

Follow me Mr Meshacking

13/06/2026

ALIKUWA MWAMINIFU SANA KWA MWANAMKE.

mwanamke huyo anaweza kuondoka kwenda mizunguko yake kisha anamuacha mtoto nyumbani huku mbwa huyo mpole, mtiifu, na mnyenyekevu akimlinda mtoto na kucheza nae na mwanamke huyo anaporudi anakuta mtoto kalala usingizi mzito pamoja na mbwa huyo.

Siku moja mwanamke alienda sokoni na k**a kawaida yake akamuacha mtoto pamoja na mbwa.
Aliporudi, aligundua kuna jambo la kutisha sana, vitu vilikuwa vimevurugika ndani hatari, mbaya zaidi mtoto hakuwa kwenye kitanda chake cha kubembea. Damu zilikuwa zimetapakaa kwenye kitanda cha mtoto na kwenye kabati yaani kwa ufupi chumba kizima kilikuwa na damu.

Mwanamke huyo alianza kumtafuta mtoto chumbani humo kila kona, Ghafla mbwa huyo akajitokeza kutoka chini ya kitanda akijilamba ulimi na akitikisa mkia na kichwa k**a umbwa alietoka kula msosi wa hatari.

Moja kwa moja mama huyo akafikiria kuwa mbwa atakuwa k**aliza kumla mtoto wake, akachukua ukuni mkubwa akampiga kipigo cha adabu mbwa huyo mpaka akamuua.

Kisha aliendelea kumtafuta mtoto wake huku akiwaza kuwa hata akipata kiungo kimoja cha mtoto wake itakuwa afadhari tu.

Ghafla tena chini ya kitanda humohumo akamuona mtoto wake akiwa salama kabisa bila kovu lolote huku akiwa na tabasamu,

Kwa hofu kubwa tena akaona nyoka wawili wakubwaaa wakiwa wanavuja damu huku vichwa vyao vikiwa vimetengana na miili. Ilikuwa ni vita kubwa kati ya nyoka hao na mbwa, na yote haya mbwa alifanya ili kuhakikisha usalama wa mtoto.

Lakini tayari kutokana na kutokuwa mvumilivu pamoja na kuwa na hasira za haraka akawa amemuua mbwa mwaminifu, mpole, mnyeyekevu.
--------------
Ni mara ngapi tunawahukumu watu kwa maneno mabaya na kuwatendea vitendo vya uovu bila kuchukua mda na kufanya tathimini????
Kwako wewe unaesoma post hii, Naomba Mungu akusamehe kwa neema yake kutokana na makosa ambayo unafanya bila kujua ama kufikiria lakini bado anakupenda na unazidi kupata neema ya uhai. Mungu atubariki.

Toa maoni yako umejifunza nini? Usisahau kuni follow Mr Meshacking

12/06/2026

NDUGU ZANGU PALE NINAPOKOSEA KATIKA POST ZANGU MNIKOSOE TU MAANA MKINIKOSOA KUNA VITU NITAJIFUNZA NA KUREKEBISHA.
Ahsanteni sana.

12/06/2026

Mr Meshacking STORY FUPI YA MFUNGWA JELA

Kulikuwa na kijana mmoja anaitwa Juma. Juma alikulia katika mazingira magumu sana, na kwa sababu ya marafiki wabaya akaingia kwenye wizi mdogo mdogo. Siku moja alik**atwa na kupelekwa jela.

Alipofika jela, maisha hayakuwa rahisi. Alikosa uhuru, chakula kilikuwa cha kawaida tu, na kila siku alilazimika kufuata sheria kali. Mwanzoni alijuta sana na alijilaumu kwa makosa yake.
Siku moja, alikutana na mfungwa mzee aliyeitwa Mzee Kondo. Mzee huyo alimshauri akasema,
"Jela si mwisho wa maisha, ni nafasi ya kubadilika."

Maneno hayo yalimgusa Juma. Akaanza kubadilika—alianza kusoma vitabu, kujifunza stadi mpya k**a useremala, na hata kuwasaidia wafungwa wenzake kusoma.
Miaka ilipita, na siku ya Juma kuachiwa ilifika. Alipotoka jela, hakuwa yule kijana wa zamani tena. Alikuwa mtu mwenye nidhamu, mwenye malengo, na mwenye ndoto mpya.

Alifungua karakana ndogo ya useremala, na baadaye akawa mfano mzuri kwa vijana wa mtaa wake, akiwaelimisha kuepuka makosa aliyoyafanya.
Mwisho wa siku, Juma aligundua kuwa kosa linaweza kubadilika kuwa somo—ukiamua kubadilika😊

Follow and like my page

12/06/2026

Salamu za kipekee kwa mashabiki bora wageni! Cotridah Patrick Haule, Kelvin Okelo, Toby Jb

10/06/2026

Mr Meshacking NANI UNAMKUBALI KATIKA UIGIZAJI?

Au ONDOKA NA MMOJA TU. 😂😂

10/06/2026

Mr Meshacking :
TAHADHARI KWA WAZAZI NA WALEZI 🛡️🏡

​Dunia ya sasa imebadilika sana, na changamoto za malezi zimekuwa kubwa kuliko vizazi vilivyopita. K**a mzazi au mlezi, jukumu lako la kwanza siyo tu kutoa chakula na mavazi, bali ni kuwa mlinzi wa kwanza wa maadili na usalama wa mtoto wako.
​Hivi sasa, kuna mmomonyoko mkubwa wa maadili unaoenea kwa kasi, hususan changamoto ya ushoga na vitendo vya kikatili dhidi ya watoto wa kiume. Ukweli ni kwamba watoto wetu wa kiume wapo hatarini, na mara nyingi adui anatumia mlango wa "urafiki wa karibu" au "mazoea" kupitia vijana wakubwa au watu wazima wanaojifanya wema.

:

:
Usiruhusu vijana wakubwa au watu baki kuingia kwenye urafiki wa karibu kupitiliza na mtoto wako mdogo bila sababu za msingi. "Mazoea ya ajabu" mara nyingi ni mwanzo wa mitego.

:
Mfundishe mtoto wako tangu akiwa mdogo kuwa mwili wake ni mali yake, na hakuna mtu anayeruhusiwa kuugusa kinyume na taratibu, hata k**a ni ndugu au rafiki wa familia.
​Kuwa Rafiki wa Mtoto: Mtengenezee mazingira ambapo akifanyiwa kitu kibaya au akiona kitu kisichoeleweka, awe huru kukuambia wewe kwanza bila uoga wa kupigwa.

:
Jua mtoto wako yuko wapi, anacheza na nani, na anatazama nini kwenye simu au TV. Mitandao imekuwa uwanja mpya wa kuharibu fikra za watoto wetu.
​Ujumbe kwa Jamii:

Usiwe mzazi wa "kujiamini kupitiliza." Kuwa mkali na makini kwa maslahi ya mwanao. Uharibifu ukishatokea, majuto hayatasaidia kurudisha utu na maisha ya mtoto huyo. Tuungane kulinda kizazi kijacho.

09/06/2026

Mr Meshacking Funguka Bila Woga Mdau Wangu.👇

09/06/2026

Mr Meshacking MAJUTO NI MJUKUU
Dada zangu kuna kitu cha kujifunza hapa!!

Niliolewa na mwanaume mpole sanaaaaaa miaka mitano iliyopita, yani nikisema mpole ni mpole mno, hakunifatilia hata siku moja, hakuniuliza nini wala nini, alinpa uhuru wa kutosha, nikiaga naenda mahali anasema nenda, hata k**a narudi saa

nane usuku atanifata tu maana hakuwa akipenda niendeshe gari usiku hata sikumoja, nikirud na tax ananifokea sana,,,, gari mafuta niliwekewa kila safari, vocha niliwekewa, alinikuta fresh from collage so hata kazi sikuwa nayo, akanitafutia kazi,baada

ya ndoa, nikapata, na nikaanza, kuna kipindi akawa ananiambia niache gari anafeele proud kutembea na mimi kwenye gari, kifupi alinijali sana, sana sana,,,,,,,, sasa ile care yake ndio ninayoikumbuka hadi leo hii, wamama, wadada, wanandoa,

K**a una mwanaume anakujal mshikilie vizuri sana. Si kwamba alikuwa hanithamini, alikuwa ananithamini sana tu, sikuwah kumfumania hata mara moja, ana likuwa muwazi sana kwangu, yani muwaz sanaaa, ofisn kwao walinijua, alipenda

kunitambulisha kila kona,,,, kuna kipindi alienda south kikazi ikawa kila weekend ananitumia nauli naenda, siku zingine anakuja yeye hadi aliporudishwa huku, ni upendo wa ajabu,, Nilichofaidi kwake tu ni kwamba alikwenda kwetu akapaona palivyo, akasema atanisaidia kujenga, alivunja nyumba ile na kumjengea mama yangu kijumba kidogo cha kumtosha mwenyewe, akamuwekea mashamba, hadi leo namkumbuka, kwao yye kazaliwa peke yake, mama yake alifariki wakati amemzaa tuu, akasema anamlea mama yangu k**a mama yake, hana dada wala kaka wa kuzaliwa tumbo moja, wako wa ndugu wengine tu

NATHIBITISHA KWA KINYWA CHANGU, COMPANY ULIYONAYO INAWEZA KUBADILI MSIMAMO NA KUSHUSHA AU KUZIDISHA HESHIMA YAKO,,, company niliyokuwa nayo mimi ilikuwa ni ya kupunguza heshima kwangu na ndio iliyoniponza, staki kuiongelea sana hilo maana wengi rafiki zangu wako humu, ila kifupi tu, nilifanya ujinga mno, naujutia hadi kesho,

Nikiwa na rafiki zangu tuliandaa mtoko kwenda bagamoyo kutembea lakini tukapanga tusiwaambie waume zetu ukweli, tudanganye maana wengi wasingekubali tukapanga safari tukasema uongo kwamba ni safari za kiofisi,( mme wangu hakuwa akinifatilia oficn kabisa) basi nikamwambia ni safar ya kikazi tunaenda bagamoyo, yeye oficn kwake ni boss, so anaweza kuondoka muda wowote bila swali, basi akasema nitakufata, sitawasumbua nitakaa hotelini tu, wewe ukimaliza kikao chenu utanikuta chumbani, nakumbuka siku hiyo nilichukia sanaaa, yani sanaaaa nilichukia nikamwambia hapana tunalala wawili wawili, akasema basi sawa nenda,

Alinipa hela ya kutosha nikaenda na rafiki zangu tulikuwa group ya watu wanne tu, watatu tumeolewa mmoja bado, basi kufika bagamoyo tuli have fun sana almost three days, nikiwa kule nikakutana na kijana mmoja ambae alinipenda sana (admin naficha jina,,,, ila tumpe KELVIN) basi alikuwa kaja na marafiki zake wengine nafikir nao kuhv fun,

Sasa kila jioni tukiiniga buffet tunakutana nae, akaanza kunitongoza nikagoma, akamfata mmoja wa rafiki zangu akaomba namba akapewa, nashangaaa usiku akanipigia simu, nikakataaa, rafiki zangu walinisisitiza sana nimkubali, kijana mzuri, handsome, nikasema no, ninae mme wangu, simtaki huyu,,,,,

Siku naondoka akaja na diary moja nzuri sana kwenye gari yetu, akaniambia unaondoka nikasema ndio unataka nini, akasema don’t be dry like this akanipa diary yake niichukue k**a kumbukumbu, nikakataa nilipofika mjin mr alinifata, akanipokea akaniambia tu mke wangu toka toka uende huko, nimekuwa mpweke sana,, wkati huo sikujua k**a alipiga simu ofisn kuconfirm k**a ni kweli niliondoka,,, akaambiwa nimejaza AD na sio kwamba nimesafiri kikazi,,, kumbe ukweli aliujua, nashangaa mwanaume huyu hakuniuliza chochote akakaa kimya tu, ila aniliona changez, coz tulipokuwa kweny gari alinikuwa ananiangalia sanaaaaaaaa,,, nikimtazama na mimi anageuka anaangalia pembeni,

Nikamuuliza vipi, akasema nilikumiss tu mke wangu,,,, tukafika home nikaoga nilikuwa nimechoka kesho asubuh tukaondoka, kila mtu na gari yake, kufika ofic hro hakuniambia chochote k**a aliwasiliana na mme wangu aliniuliza tu, umepona? Nikasema ndio akasema karibu tena, basi kazi ikaendelea,,,,,,

Baada ya siku nne tu akaja yule kaka hado oficn kwangu na alielekezwa na mmoja wa hao best zangu, alipofika nilishangaa nikamuuliza nini kimekuleta hapa akasema tuongee kwenye gari, basi nikaingia, jamani ni k**a nililogwa naweza sema kweli tena, k**a hamtaamin basi ila naamini ALINIROGA HUYU KAKA, maana alivyokwua akiongea nikaanza kumpenda,,, nilizidi kumpenda kupita kiasi nikaanzak uona uzuri wkae, nikaanza kumcompare na franco wangu, naona huyu amemzidi kila kitu,

✍️K**a umeipenda andika ENDELEA ..

Baadae aliniaga akasepa, tokea pale nikaanza kumpenda kupita maelezo .. ITAENDELEA...

Want your public figure to be the top-listed Public Figure in Arusha?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Arusha